-
Sudan yatangaza janga la kipindupindu baada ya mvua kubwa kunyesha nchini humo
Aug 18, 2024 03:34Waziri wa Afya wa Sudan ametangaza janga la kipindupindu nchini humo baada ya mvua kubwa kunyesha kwa wiki kadhaa.
-
Udhalilishaji wa kingono watumiwa kama silaha ya vita katika mzozo huko Sudan
Aug 17, 2024 22:58Pande husika katika vita vya ndani nchini Sudan zimetekeleza udhalilishaji wa kingono na vitendo vingine vya unyanyasaji kama silaha ya vita tangu kuanza mapigano ya ndani nchini humo mwezi Aprili mwaka jana.
-
Waliokufa kutokana na mvua, mafuriko Sudan wapindukia 50
Aug 11, 2024 04:04Watu zaidi ya 50 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 200 kujeruhiwa kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha na kusababisha mafuriko katika maeneo mbali mbali ya Sudan.
-
WHO: Vita vimefanya tuluthi 2 ya Wasudan washindwe kutafuta matibabu
Aug 09, 2024 03:48Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) amesema thuluthi mbili ya wananchi wote wa Sudan hawawezi kutafuta huduma za matibabu kutokana na mgogoro na vita vinavyoendelea kushuhudiwa nchini humo.
-
Mafuriko kaskazini mwa Sudan yaua na kujeruhi makumi ya watu
Aug 06, 2024 23:50Shirika rasmi la Habari la Sudan (SUNA) limeripoti kuwa watu 11 wamefariki dunia na wengine 60 kujeruhiwa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha na kusababisha mafuriko katika mji wa Abu Hamad kaskazini mwa Sudan. Mvua hiyo imebomoa makumi ya nyumba huku timu za uokoaji zikiendelea kusaka watu waliotoweka na wengine walionasa chini ya vifusi.
-
FAO: Hatua za haraka zichukuliwe kukabiliana na njaa katika baadhi ya maeneo ya Darfur
Aug 05, 2024 23:26Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) limetoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka baada ya tatizo la njaa kuyaathiri baadhi ya maeneo ya Darfur. Shirika la FAO limeeleza haya katika ripoti yake ya karibuni kuhusu tathmini ya usalama wa chakula.
-
Mkuu wa jeshi la Sudan Abdel-Fattah al Burhan anusurika katika jaribio la mauaji
Jul 31, 2024 08:19Jeshi la Sudan limetangaza kuwa kamanda wake mkuu, Jenerali Abdel-Fattah al Burhan amenusurika katika shambulio la ndege mbili sisizo na rubani (droni) katika hafla ya wahitimu wa jeshi. Watu watano wameuawa katika hujuma hiyo ya droni mashariki mwa Sudan.
-
HRW: Pande hasimu Sudan zimeshiriki katika ukatili mkubwa wa kijinsia
Jul 29, 2024 22:59Pande zinazozozana huko Sudan zimeshiriki katika ukatili mkubwa wa kingono na kijinsia katika mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum.
-
Shambulio la RSF laua watu 22 el-Fasher, magharibi mwa Sudan
Jul 28, 2024 03:23Kwa akali watu 22 wameuawa katika shambulio linalodaiwa kufanywa na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) katika mji wa el-Fasher, jimboni Darfur, magharibi mwa Sudan.
-
Mvua kubwa yazidisha mateso ya wakimbizi mashariki mwa Sudan
Jul 27, 2024 03:32Mvua kubwa inayoendelea kunyesha huko mashariki mwa Sudan imezidisha mateso ya watu waliokimbia makazi yao haswa katika miji ya Gedaref, Kassala na Halfa Aj Jadeedah.