-
AU yataka pande hasimu Sudan zisitishe mapigano
Dec 19, 2023 23:34Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ametoa mwito kwa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) na Jeshi la Sudan kusitisha uhasama na mapigano mara moja, na kwenda kwenye meza ya mazungumzo kwa shabaha ya kurejesha utulivu, uthabiti na amani endelevu katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Mapigano nchini Sudan yapanuka hadi Wad Madani, maelfu ya watu wahama makazi yao
Dec 17, 2023 07:51Shirika la habari la Reuters limeripoti kuwa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vinapigana na Jeshi la Sudan nje ya mji wa Wad Madani katika Jimbo la Al-Jazira (katikati mwa Sudan) na kwamba mapigano hayo yamelazimisha maelfu ya raia kukimbia makazi yao na kuelekea maeneo salama.
-
UN yaiondoea vikwazo vya silaha Somalia, yahitimisha shughuli zake za kisiasa nchini Sudan
Dec 02, 2023 02:29Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha kwa kauli moja azimio la kuondoa vikwazo vya mwisho vya silaha dhidi ya serikali ya Somalia na vikosi vyake vya usalama, huku likihitimisha pia shughuli za ujumbe wake wa kisiasa katika nchi ya Sudan iliyokumbwa na vita.
-
UN yatoa indhari: Idadi ya wanaokimbilia Sudan Kusini kutoka Sudan imeongezeka
Nov 10, 2023 03:26Mashirika ya kibindamu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini yametahadharisha kuhusu ongezeko kubwa la watu wanaorejea na wakimbizi wanaokimbia mzozo na kuelekea kaskazini nchini Sudan.
-
Familia za Wasudan zatafuta hifadhi Sudan Kusini
Oct 27, 2023 09:39Ripoti zinasema kuwa katika hali ya kusikitisha, familia zinazoepuka ghasia na machafuko nchini Sudan zinaendelea kuwasili katika maeneo ya mbali ya kaskazini mwa Sudan Kusini.
-
UNHCR: Watu elfu nne wameuliwa Darfur, Sudan, mali za raia zimeharibiwa
Oct 18, 2023 00:20Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema, watu wapatao 4,000 wameuawa huku mali za raia zikiharibiwa katika mapigano yanayoendelea huko jimboni Darfur nchini Sudan, mapigano ambayo yalianzia kwenye mji mkuu Khartoum miezi sita iliyopita na kusambaa hadi nje ya mji huo, kati ya Jeshi la Serikali (SAF) na wanamgambo wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF).
-
Salva Kiir kuwa mwenyeji wa viongozi wa Sudan kujadili amani
Oct 17, 2023 10:42Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir amesema karibuni hivi atakuwa mwenyeji wa mkutano utakaowaleta pamoja viongozi wa pande mbili zinazopigana nchini Sudan, yaani Jeshi la Taifa la Sudan (SAF) na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF)
-
Iran na Sudan kufungua tena balozi zao baada ya kukamilisha mchakato wa kuhuisha uhusiano
Oct 10, 2023 03:34Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, karibuni hivi Iran na Sudan zitafungua tena balozi zao baada ya nchi hizo mbili kukamilisha mchakato wa kurejesha uhusiano wa kidipolmasia.
-
UN: Mapigano Sudan yanasababisha kuongezeka kwa kasi mgogoro wa wakimbizi duniani
Oct 05, 2023 23:57Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu huko Sudan amesema kuwa mapigano yanayoendelea nchini humo yanapelekea kuongezeka haraka mgogoro unapanuka wa wakimbizi duniani.
-
Sudan Kusini: Benki ya BRICS ni mwanzo wa mwisho wa udhibiti wa sarafu ya dola
Sep 30, 2023 12:14Waziri wa Mambo ya Rais wa Sudan Kusini amesema kuwa, kudhihiri kwa Benki mpya ya NDB ya kundi la madola yanayoinukia kiuchumu la BRICS utakuwa mwanzo wa kusambaratika udhibiti wa sarafu ya dola ya Marekani katika miamala ya kifedha duniani kote.