-
Mawaziri wanne muhimu wa serikali ya mpito Sudan wapigwa kalamu nyekundu
Jul 09, 2020 21:56Waziri Mkuu wa Sudan Abdalla Hamdok amewabadilisha mawaziri wanne na maafisa wengine waandamizi watatu wanaoongoza wizara za serikali ikiwa ni sehemu ya mabadiliko makubwa aliyotangaza kuyafanya katika baraza la mawaziri la serikali hiyo ya mpito anayoiongoza.
-
Serikali ya mpito Sudan yampiga kalamu nyekundu Mkuu wa Jeshi la Polisi na Naibu wake
Jul 06, 2020 06:21Serikali ya mpito ya Sudan imetangaza kuwa imemwachisha kazi mkuu wa jeshi la Polisi na naibu wake, siku chache baada ya kufanyika maandamano makubwa ya kutaka hatua zaidi zichukuliwe dhidi ya maafisa wenye mfungamano na aliyekuwa rais wa nchi hiyo aliyeondolewa madarakani, Omar al-Bashir.
-
Waziri Mkuu Sudan aahidi kutimiza matakwa ya Wasudan katika wiki mbili zijazo
Jul 05, 2020 09:53Waziri Mkuu wa Sudan amesema kuwa amekutana na makundi mbalimbali ya kisiasa na kijamii katika siku chache zilizopita na kupokea miito inayomtaka asahihishe mwelekeo wa serikali yake na kutimiza malengo ya mapinduzi ya Wasudani yaliyomuondoa madarakani rais wa zamani wa nchi hiyo, Omar al Bashir.
-
Waasi wa SPLM nchini Sudan watangaza kusitisha vita kwa miezi saba
Jul 02, 2020 07:56Tawi la kaskazini la kundi la waasi la SPLM la Sudan limetangaza kuongeza muda wa kusitisha vita kwa miezi mingine saba.
-
Nchi za Sahel Afrika zaomba kufutiwa madeni yote kwa ajili ya kukabiliana na ugaidi
Jul 01, 2020 06:52Mkutano wa nchi Sahel Afrika na Ufaransa umetoa wito wa kufutwa madeni yote ya nchi hizo ili kusaidia juhudi za kupambana na athari mbaya zilizosababishwa na mlipuko wa maambukizi ya virusi vya corona, mapambano dhidi ya ugaidi na mikakati ya ustawi na maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
-
Watu wa Sudan waandamana wakitaka mabadiliko ya haraka
Jun 30, 2020 22:00Wananchi wa Sudan wameandamana katika mji mkuu, Khartoum na miji mingine ya nchi hiyo wakitaka mabadiliko ya haraka na haki kwa waliouawa katika maandamano ya mwaka jana yalyopelekea jeshi kumuondoa madarakani mtawala wa muda mrefu Omar al-Bashir.
-
Mgogoro wa Bwawa la Renaissance waingia Baraza la Usalama, Ethiopia yatahadharisha
Jun 29, 2020 23:15Mgogoro wa Bwawa la Renaissance (Al Nahdha) baina ya Misri, Sudan na Ethiopia umewekwa rasmi kwenye meza ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa baada ya Misri kuwasilisha muswada huo kwa ajili ya kujadiliwa na wanachama wa baraza hilo.
-
Ethiopia: Marekani ikome kuiunga mkono Misri kibubusa
Jun 28, 2020 23:26Gazeti moja la Ethiopia limeishambulia vikali serikali ya Marekani kwa kile lilichosema ni uungaji mkono wa kibubusa na kipofupofu wa misimamo ya Misri katika mazungumzo ya kutafuta suluhisho la bwawa na al Nahdha linalojengwa na Addis Ababa juu ya maji ya Nto Nile.
-
Kuongezeka jitihada za kutatua mgogoro wa bwawa la al Nahdha
Jun 27, 2020 09:12Hitilafu zinazoendelea baina ya nchi za Misri, Sudan na Ethiopia kuhusu ujenzi wa bwawa na al Nahdha juu ya maji ya Mto Nile na mgogoro uliosababishwa na hitilafu hizo zimezidisha jitihada za kikanda na kimataifa za kutafuta suhulisho la hitilafu hizo.
-
Baraza la Utawala Sudan laahidi kuitisha uchaguzi huru na wa haki
Jun 18, 2020 03:47Naibu Mkuu wa Baraza la Utawala nchini Sudan ameahidi kuwa serikali ya Khartoum itaitisha uchaguzi mkuu huru na wa wazi.