-
Ndejembi aapishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Aug 29, 2026 10:46Deogratius Ndejembi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameapishwa kushika wadhifa huo mbele ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma.
-
Ndejembi apitishwa kwa 100% kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Aug 28, 2026 14:37Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limempitisha Deogratius John Ndejembi kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kupata kura zote 324 zilizopigwa, sawa na asilimia 100.
-
Dakta Nchimbi atangaza kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais wa Tanzania
Aug 25, 2026 13:33Dakta Nchimbi atangaza kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais wa Tanzania
-
Rais Samia azindua mradi mkubwa utakaochangia nusu ya umeme unaozalishwa Tanzania
Aug 22, 2026 13:10Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amezindua Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere, hatua inayofungua rasmi kuanza kwa kazi ya mojawapo ya miradi mikubwa zaidi ya miundombinu nchini humo na mradi mkubwa zaidi wa kuzalisha umeme unaofadhiliwa na serikali.
-
Jeshi la Uingereza kufanya mazoezi Tanzania baada ya mzozo na Kenya kuhusu jinai za askari
Jul 25, 2026 03:05Uingereza imefuta zoezi kubwa la kijeshi nchini Kenya baada ya pande hizo mbili kushindwa kutatua mzozo kuhusu mamlaka ya Nairobi ya kuwafungulia mashtaka wanajeshi wa Uingereza wanaotuhumiwa kutenda uhalifu katika taifa hilo la Afrika Mashariki.
-
Maridhiano ya kisiasa Zanzibar yaja na matumaini mapya
Jul 11, 2026 02:35Maridhiano mapya ya kisiasa kati ya vyama vikuu vya Zanzibar, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo, yalifikiwa rasmi jana baada ya viongozi wa pande hizo mbili kusaini tamko la pamoja.
-
Rais Samia: Russia inashiriki katika juhudi za maendeleo Afrika
Jun 11, 2026 03:06Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa Russia ina nia ya kusaidia Afrika kujenga mpangilio mpya wa uchumi wa dunia na inaendelea kujitolea kuunga mkono maendeleo ya bara hilo.
-
UN: Wakimbizi wa Burundi walioko Tanzania wanarudi makwao kwa hiari, hawashurutishwi
Feb 27, 2026 03:27Afisa wa Uhusiano wa Nje wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR nchini Tanzania Bahia Egeh amesema, wakimbizi wa Burundi walioko nchini humo ambao wanarudi makwao, wanafanya hivyo kwa hiari wala hawashurutishwi.
-
Tanzania yatoa tahadhari ya kuongezeka maambukizi ya mafua, Covid 19 na Dengue
Feb 26, 2026 00:14Wizara ya Afya ya Tanzania imetoa tahadhari ya afya kwa umma ya kuongezeka kwa maambukizi ya mafua na Uviko-19 na kuongezeka kwa hatari ya homa ya dengue, huku ikiwataka wananchi kuchukua hatua za haraka za kujikinga hasa katika kipindi cha msimu wa mvua.
-
Tanzania kuanza kujenga bandari yenye thamani ya dola bilioni 10 mwezi Desemba
Nov 24, 2025 11:44Tanzania itaanza ujenzi wa bandari mpya mashariki mwa nchi mwezi Desemba mwaka huu na hivyo kumaliza muongo mmoja wa ucheleweshaji kutokana na pingamizi la serikali kwa masharti ya awali ya kandarasi.