-
UN: Wakimbizi wa Burundi walioko Tanzania wanarudi makwao kwa hiari, hawashurutishwi
Feb 27, 2026 06:57Afisa wa Uhusiano wa Nje wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR nchini Tanzania Bahia Egeh amesema, wakimbizi wa Burundi walioko nchini humo ambao wanarudi makwao, wanafanya hivyo kwa hiari wala hawashurutishwi.
-
Tanzania yatoa tahadhari ya kuongezeka maambukizi ya mafua, Covid 19 na Dengue
Feb 26, 2026 03:44Wizara ya Afya ya Tanzania imetoa tahadhari ya afya kwa umma ya kuongezeka kwa maambukizi ya mafua na Uviko-19 na kuongezeka kwa hatari ya homa ya dengue, huku ikiwataka wananchi kuchukua hatua za haraka za kujikinga hasa katika kipindi cha msimu wa mvua.
-
Tanzania kuanza kujenga bandari yenye thamani ya dola bilioni 10 mwezi Desemba
Nov 24, 2025 15:14Tanzania itaanza ujenzi wa bandari mpya mashariki mwa nchi mwezi Desemba mwaka huu na hivyo kumaliza muongo mmoja wa ucheleweshaji kutokana na pingamizi la serikali kwa masharti ya awali ya kandarasi.
-
Rais Samia: Ghasia za uchaguzi zinaweza kuathiri upatikanaji wa fedha
Nov 19, 2025 06:58Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania jana alisema kuwa ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi wa Oktoba 29 zinaweza kuathiri upatikanaji wa ufadhili wa kimataifa kwa nchi hiyo.
-
Vyombo vya usalama Tanzania vyamkamata raia wa Marekani na Kenya akiwa na mabomu
Nov 17, 2025 03:46Polisi ya Tanzania imetangaza kuwa imemkamata raia wa Marekani na Kenya akiwa na mabomu katika mpaka wa Tanzania na Kenya.
-
Bunge la Tanzania lamthibitisha Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa nchi hiyo
Nov 13, 2025 13:50Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Alhamisi limemthibitisha Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa nchi hiyo baada ya kupata kura 369 kati ya kura 371 zilizopigwa na wabunge. Baada ya uthibitisho huo, Dkt. Nchemba ataapishwa na Rais Samia Suluhu Hassan na kuanza mara moja majukumu yake.
-
Watu 145 washtakiwa kwa uhaini wakidaiwa kuhusika katika maandamano ya vurugu Tanzania
Nov 08, 2025 04:07Waendesha mashtaka nchini Tanzania jana Ijumaa wamewashtaki takriban watu 145 kwa kosa la uhaini madai ya kuhusika katika maandamano ya vurugu yaliyozuka wakati wa uchaguzi wa rais na bunge wiki iliyopita.kulingana na faili za mahakama zilizoonekana na Reuters.
-
Kenya yataka majibu kwa Tanzania kuhusu raia wake waliokumbwa na misukosuko ya baada ya uchaguzi
Nov 07, 2025 11:51Kenya imeitaka Tanzania itoe majibu kuhusu hali ya raia wake waliojipata kwenye mzozo wa baada ya uchaguzi, huku ikishinikiza serikali ya nchi hiyo ihakikishe usalama wao na kuchukua hatua dhidi ya ukiukaji wa haki zao.
-
Waangalizi wa AU: Uchaguzi wa Tanzania haukukidhi viwango vya kimataifa
Nov 06, 2025 11:12Ujumbe wa waangalizi wa Umoja wa Afrika katika uchaguzi mkuu wa wiki iliyopita nchini Tanzania uliogubikwa na ghasia umeeleza kuwa uchaguzi huo haukukidhi viwango vya kimataifa vya kidemokrasia.
-
Wananchi wa Tanzania wanaendelea kusubiri matokeo ya uchaguzi
Oct 30, 2025 13:01Wananchi wa Tanzania wanaendelea kusubiri matokeo ya uchaguzi uliofanyika jana Jumatano na kutawaliwa na maandamano ya hapa na pale huku hali ya mambo ikianza kurejea katika hali ya kawaida.