-
Ayatullah Kashani: Taifa la Iran halitasalimu amri mbele ya mashinikizo ya maadui
Mar 15, 2019 12:17Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema maadui wamekuwa wakitumia njama mbalimbali kama za kiuchumi, kisiasa, kijamii na kiutamaduni ili kutoa pigo kwa mfumo wa Kiislamu unaotawala hapa nchini Iran, lakini amesisitiza kuwa, katu taifa kubwa la Iran haliwezi kusalimu amri mbele ya mashinikizo ya maadui.
-
Mkutano wa Umoja wa Kiislamu, Iran iko mstari wa mbele katika kambi ya kupigania uhuru
Nov 25, 2018 12:43Mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu unaendelea hapa mjini Tehran kwa kaulimbiu ya "Quds, Nguzo ya Umoja wa Umma". Mkutano huo wa siku tatu unahudhuriwa na shakhsia 300 wa kisiasa na kidini kutoka nchi mbalimbali duniani na unajadili njia za kutatua matatizo ya ulimwengu wa Kiislamu.
-
Haniya: Malengo ya Palestina ni suala la umma wote wa Kiislamu
Nov 24, 2018 10:13Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amehutubu katika Kongamano la Kimataifa la Umoja wa Kiislamu mjini Tehran na kusema: "Utawala wa Kizayuni ni adui mkuu wa Umma wa Kiislamu."
-
Kikao cha Tehran chalaani kuwa na uhusiano wa kawaida na Israel
Nov 23, 2018 23:16Taarifa ya mwisho ya kikao cha "Nafasi ya Vyama na Wanaharakati wa Kisiasa katika Kupunguza Hitilafu za Kimadhehebu na Kulinda Malengo ya Palestina" kilichofanyika hapa mjini Tehran imelaani hatua ya baadhi ya nchi za Kiarabu ya kuwa na uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel na imesisitizia udharura wa kulindwa Quds na Palestina kwa nguvu zote.
-
Louis Farrakhan, kiongozi wa harakati ya Nation of Islam ya Marekani amuonya Trump
Nov 08, 2018 11:12Louis Farrakhan, kiongozi wa harakati ya Kiislamu ya Nation of Islam ya nchini Marekani amemtahadharisha vikali rais wa nchi hiyo Donald Trump kwamba asithubutu kuanzisha vita katika eneo la Mashariki ya Kati kwa kushinikizwa na utawala haramu wa Israel, akisisitiza kuwa matokeo ya vita hivyo yatakuwa mabaya mno.
-
"Uwezo wa kujihami Iran ni kwa maslahi ya kuzuia vita Mashariki ya Kati"
Oct 26, 2018 11:49Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amesema stratijia ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kuimarisha uwezo wake wa kujihami ni kwa shabaha ya kuzuia vita katika eneo hili la Mashariki ya Kati.
-
Zarif: Mapatano ya kumaliza ugaidi na mateso ya wananchi wa Idlib Syria yameshafikiwa
Sep 07, 2018 20:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, katika kikao cha pande tatu za Iran, Russia na Uturuki kilichofanyika hapa Tehran jana Ijumaa, kumefikiwa mapatano ya kumaliza ugaidi na mateso ya wananchi wa mkoa wa Idlib, nchini Syria.
-
Taarifa ya pamoja ya marais wa Iran, Russia na Uturuki kuhusu Syria katika kikao cha Tehran
Sep 07, 2018 10:37Marais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Russia, na Uturuki wametoa taarifa ya pamoja baada ya mkutano wao wa pande tatu mjini Tehran ambapo wamesisitiza kuhusu msimamo wao wa kudumishwa uhuru, mamlaka ya kujitawala na kulinda mipaka yote ya Syria.
-
Qassemi: Kikao cha Tehran ni fursa nzuri kwa ajili ya muungano wa kieneo
Sep 06, 2018 03:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa kikao cha wakuu wa Iran, Uturuki na Russia hapa Tehran ni fursa nzuri kwa diplomasia na mchakato wa kisiasa wa kuvishinda vita na magaidi kusalimu amri mbele ya matakwa na irada ya wananchi.
-
Siddiqui: Iran haitafanya mazungumzo na serikali na rais wa sasa Marekani
Aug 03, 2018 11:08Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo mjini Tehran amesema Wamarekani si watu wa kufanya nao mazungumzo na iwapo kuna siku Iran itafanya mazungumzo basi si na rais na serikali ya sasa ya Marekani.