-
Aliachwa akihangaika na kifo peke yake; Hasira zatanda Ufaransa baada ya kifo cha mwanafunzi mwenye asili ya Kiarabu
Mar 24, 2023 22:50Mitandao ya kijamii nchini Ufaransa imeshuhudia wimbi kubwa la hasira na ghadhabu baada ya kifo cha mwanafunzi mwenye asili ya Kiarabu ambaye alipatwa na mshtuko wa moyo, huku kukiwa na shutuma kwamba uongozi wa shule ulimwacha akikabilina na kifo peke yake bila ya kumpa huduma ya dharura.
-
Ubaguzi washadidisha mgogoro wa 'afya ya umma' Marekani
Jan 10, 2023 04:22Miji na kaunti zaidi ya 200 nchini Marekani zimeutangaza ubaguzi wa rangi nchini humo kama mgogoro wa afya ya umma. Wataalamu wa afya wameonya kuwa, ubaguzi wa kimfumo wa miongo kadhaa umeendelea kuathiri afya za Wamarekani wasio wazungu.
-
Taasisi ya utafiti: Uingereza inatunga sheria za kuwafanya Waislamu kuwa raia wa daraja la pili
Sep 12, 2022 21:59Taasisi ya Mahusiano ya Mbari ya Uingereza (The Institute of Race Relations) imesema, sera ya serikali ya Uingereza inawafanya Waislamu wa nchi hiyo kuwa raia wa daraja la pili kutokana na sheria zinazoruhusu kupokonywa uraia wa Uingereza.
-
Kanisa la Kiprotestanti la Marekani: Israeli ni dola la ubaguzi wa rangi (apartheid)
Jul 10, 2022 03:43Mkutano Mkuu wa Kanisa la Kiprotestanti la Presbyterian la Marekani, huko Louisville, Kentucky, umepiga kura kwa wingi wa asilimia 70 ukiunga mkono azimio la kuitangaza Israeli kama dola la ubaguzi wa rangi.
-
Afisa wa Iran: Ubaguzi umekita mizizi katika historia ya Uingereza
Jun 22, 2022 23:08Ubaguzi na udhalilishaji wa binadamu ni mambo yaliyokita mizizi katika historia ya Uingereza. Hayo yamesemwa na Katibu wa Baraza Kuu la Haki za Binadamu la Iran, Kazem Gharibabadi katika ujumbe wake kwa njia ya Twitter.
-
Rais wa Afrika Kusini alaani hujuma dhidi ya raia wa kigeni
Apr 11, 2022 22:11Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini amesema ni jambo la kusikitisha kuona kuwa hisia na hujuma dhidi ya raia wa kigeni zinashabihiana na yale yaliyokuwa yakijiri nchini humo katika zama za utawala wa ubaguzi wa rangi au apathaidi.
-
Waislamu India wakasirishwa na uamuzi wa mahakama ulioidhinisha matamshi ya chuki
Mar 30, 2022 07:18Wimbi la kejeli na hasira limetanda katika mitandao ya kijamii nchini India baada ya mahakama kufunga kesi dhidi ya wanasiasa wawili waliotoa matamshi ya kichochezi dhidi ya Waislamu, ikisema kuwa uchochezi si kauli za chuki ukiambatana na tabasamu.
-
Abbas akosoa undumakuwili wa nchi za Magharibi kuhusu vita vya Russia na Ukraine
Mar 28, 2022 21:01Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina (PA) Mahmoud Abbas amezikemea nchi za Magharibi kwa kutumia sera za kinafiki na kindumakuwili baada ya kuchukua hatua kali dhidi ya Russia kuhusu operesheni yake ya kijeshi nchini Ukraine huku zikipuuza uhalifu unaofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Ripoti ya Chuo Kikuu cha Harvard yalaani uvamizi na uhalifu wa ubaguzi wa rangi wa Israel huko Palestina
Mar 22, 2022 08:23Ripoti ya Kituo cha Haki za Binadamu cha Harvard imeibua hasira miongoni mwa maafisa wa utawala haramu wa Israel na duru zinazoiunga mkono Tel Aviv, baada kulaani uvamizi wa utawala huo huko Palestina ikiutaja kuwa ni "uhalifu wa ubaguzi wa rangi, apartheid."
-
Ripoti ya Mkaguzi Mkuu: 47% ya Wafanyikazi wa Hospitali ya Rufaa ya Kenyatta wanatoka kabila moja
Mar 10, 2022 11:03Ripoti mpya inaonyesha kuwa kabila moja linaunda karibu nusu ya wafanyikazi wa Hospitali ya Rufaa na Utafiti ya Chuo Kikuu cha Kenyatta (KUTRRH nchini Kenya.