Data zilizotolewa na Kituo cha Takwimu cha Ulaya cha Eurostat zimefichua kuwa, Ujerumani imeagiza shehena kubwa ya mafuta kutoka Iran kwa mara ya kwanza tokea mwaka 2018, licha ya vikwazo vya Marekani.
Matokeo ya utafiti uliofanyika nchini Ujerumani yanaonyesha kuwa zaidi ya theluthi moja ya wanaume nchini humo wanaona kuwa unyanyasaji dhidi ya wanawake "unakubalika".
Idara ya Kuzuia Uhalifu ya Ujerumani imetangaza kwamba makumi ya mashambulizi dhidi ya misikiti yamesajiliwa nchini humo mwaka 2022.
Kansela Olaf Scholz wa Ujerumani amesema nchi yake inaunga mkono mpango wa bara la Afrika kuwa na uwakilishi wa kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Filamu ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii imemuonyesha mtoto mdogo wa Kiislamu akiondolewa kwa nguvu katika familia yake ya Kiislamu na maafisa wa "huduma za ulinzi wa watoto" wakisaidiwa na askari polisi wa Ujerumani. Maafisa wa Ujerumani wanadai kuwa wazazi wa mtoto huyo wamekuwa wakimfundisha kwamba mahusiano ya kingono ya watu wa jinsia moja hayakubaliki katika Uislamu.
Filamu ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii imemuonyesha mtoto mdogo wa Kiislamu akiondolewa kwa nguvu katika familia yake ya Kiislamu na maafisa wa "huduma za ulinzi wa watoto" na askari polisi wa Ujerumani kwa sababu wazazi wake wanadaiwa kumfundisha kwamba mahusiano ya kingono ya watu wa jinsia moja hayakubaliki katika Uislamu.
Matumizi ya kijeshi barani Ulaya katika mwaka ulipoita wa 2022 yalipita kiwango hata cha kipindi zilipomalizika enzi za Vita Baridi.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amejibu matamshi ya uingiliaji kati ya viongozi wa Ujerumani kuhusu hukumu iliyotolewa hapa nchini dhidi ya kiongozi wa kundi la kigaidi la "Tondar" na kueleza kuwa: Iran haitamuomba yoyote ruhusa katika mapambano yake dhidi ya ugaidi na kutekeleza uadilifu dhidi ya magaidi.
Mbunge mmoja wa Ujerumani ametoa mito wa kufukuzwa nchini humo vikosi vya jeshi la Marekani ambavyo vimekuwepo nchini humo kwa karibu miongo minane.
Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya China imelalamikia vikali safari ya Bettina Stark-Wattsinger, Waziri wa Elimu wa Ujerumani katika Kisiwa cha Taiwan na kusisitiza kuwa inapinga safari rasmi ya waziri huyo katika kisiwa hicho kinachomilikiwa na serikali ya Beijing.