Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limelaani vikali hatua ya mahakama ya Bahrain kudhinisha marufuku ya chama kikuu cha upinzani nchini humo, al-Wefaq.
Katika siku za karibuni, maeneo mbalimbali ya Bahrain yamekuwa uwanja wa maandamano na mikusanyiko ya wananchi ya kupinga utawala wa kidikteta wa Aal Khalifa na waungaji mkonio wake wakuu, yaani utawala wa Aal Saud.
Sheikh Issa Qassim mwanazuoni wa ngazi za juu wa Kiislamu nchini Bahrain ametoa ujumbe na kuuonya vikali ukoo wa Aal Khalifa unaotawala nchini humo kuhusu sera zake za kuzidisha mashinikizo dhidi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia wanaodhulumiwa nchini humo.
Maulamaa wa Bahrain wametaka shakhsia wa kidini na wa kisiasa wanaoshikiliwa kwenye jela za utawala wa nchi hiyo wa Aal Khalifa waachiliwe huru.
Maelfu ya Wabahrain wameendelea kufanya mgomo wa kuketi chini mbele ya nyumba ya Kiongozi wa Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini huyo, Ayatullah Isa Qasim kwa siku ya nane mfululizo huku wakipiga nara zinazopinga utawala wa kifalme wa nchi hiyo.
Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu imelaani hatua ya utawala wa Aal-Khalifa kumvua uraia mwanachuoni mashuhuri wa Kiislamu nchini Bahrain Ayatullah Sheikh Isa Qassim.
Utawala wa kizazi cha Aal Khalifa nchini Bahrain umeendeleza ukiukaji wake mkubwa wa haki za binadamu kwa kumnyang'anya uraia mwanazuoni mkubwa na mashuhuri wa Kiislamu nchini humo Ayatullah Issa Ahmad Qasim.
Maulamaa wa Bahrain wametangaza kuwa hatua ya utawala wa Aal Khalifa ya kuzifuta na kuzipiga marufuku jumuiya na asasi za upinzani, kufunga ofisi zao na kuwatia nguvuni watu ni sawa na "kutangaza vita".
Mfalme wa Bahrain amepiga marufuku shughuli za kisiasa za wanazuoni nchini humo lengo likiwa ni kushadidisha ukandamizaji kwa malalamiko ya raia wa nchi hiyo.
Mfalme wa Bahrain ametoa dikrii ya kubadilishwa baadhi ya vipengee vya kisheria kuhusu vyama vya kisiasa.