-
Ushindi wa Muqawama katika uchaguzi wa Lebanon wawatia kiwewe Wazayuni
May 08, 2018 22:26Vyombo vya habari utawala wa Kizayuni wa Israel vimetangaza kuwa ushindi wa mrengo unaoongozwa na Hizbullah katika uchaguzi wa bunge la Lebanon unatia wasiwasi mkubwa.
-
Hamas: Mapambano yataendelea hadi pale utawala wa Kizayuni utakapoangamizwa
May 07, 2018 02:12Kiongozi wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kuwa, mapambano dhidi ya adui Mzayuni yataendelea mpaka pale utawala wa Kizayuni wa Israel utakapoangamizwa.
-
Rouhani: Wananchi wa Iran wako pamoja dhidi ya Trump na utawala wa Kizayuni
May 06, 2018 03:27Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa wananchi wa Iran wako pamoja dhidi ya Rais wa Marekani na utawala wa Kizayuni na kutilia mkazo kuwa wananchi wa Iran hawapendi vita, lakini wanajilinda na kujitetea kwa dhati.
-
Mwanahistoria mashuhuri wa Kiyahudi: Marekani imewafanyia hadaa watu wa Palestina
May 03, 2018 10:39Mwanahistoria mtajika wa Kiyahudi Ilan Pappé ameashiria jinsi baadhi ya Wapalestina walivyodhani kwamba Marekani ikiwa kama mpatanishi itasaidia mpango wa kuundwa nchi ya Palestina na kubainisha kuwa serikali za Marekani ikiwemo ya Barack Obama zimewafanyia hadaa watu wa Palestina.
-
Mayahudi wa Orthodox waandamana Quds (Jerusalem) na kuichoma moto bendera ya Israel
May 03, 2018 09:57Mayahudi wa Orthodox wamefanya maandamano usiku wa kuamkia leo huko katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) na kuchoma moto bendera za utawala huo katili.
-
Iran yaitaka Israel na waungaji mkono wake waache chokochoko zao la sivyo watajuta
May 01, 2018 23:17Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameuonya utawala haramu wa Israel na waungaji mkono wake na kuwataka waache njama na miamala yao hatari kwani jibu la Iran litakuwa la kushtukiza na la kuwafanya wajute.
-
Walowezi wa Kizayuni wauhujumu Msikiti wa Al Aqsa
Apr 30, 2018 09:24Makumi ya walowezi wa Kizayuni leo asubuhi Jumatatu wameuhujumu Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel.
-
Ehud Olmert: Israel haina ubavu wa kukabiliana na Iran
Apr 30, 2018 03:25Waziri Mkuu wa zamani wa utawala wa Kizayuni wa Israel amesema kuwa, utawala huo hauna ubavu wa kukabiliana na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Saeb Erekat: Hatutoshiriki katika mpango wa mapatano utakaopendekezwa na Trump
Apr 29, 2018 22:10Katibu wa kamati ya utendaji ya Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) ametangaza kuwa, Wapalestina hawatashiriki katika mpango wowote ule wa mapatano utakaopendekezwa na rais wa Marekani, Donald Trump.
-
Nabih Berri atahadharisha kuhusu Israel kuishambulia Lebanon
Apr 29, 2018 10:39Spika wa Bunge la Lebanon ametahadharisha kwamba, utawala haramu wa Israel umeajiandaa kuishambulia kijeshi nchi hiyo ya Kiarabu.