-
Wahajiri 30 wafa maji baada ya boti kuzama pwani ya Djibouti
Jan 30, 2019 11:04Maiti 30 zimepatikana zikielea majini baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya wahajiri kuzama katika pwani ya Djibouti.
-
Wahajiri 117 wahofiwa kufa maji katika pwani ya Libya
Jan 20, 2019 04:22Wahajiri zaidi ya 100 wanahofiwa kupoteza maisha katika ajali ya kuzama boti katika pwani ya Libya.
-
Wahajiri waendelea kuwa wahanga wa sera za kuwapiga vita wahamiaji za Trump
Jan 19, 2019 03:09Sera za kupiga vita wahajiri za Rais Donald Trump wa Marekani zimeendelea kutesa na kuwatia mashakani mamia ya watu baada ya polisi wa mpakani wa jimbo la New Mexico huko kusini magharibi mwa Marekani kuwatia nguvuni zaidi ya wahajiri 340 katika kituo cha mpakani cha Antelope Wells.
-
UNHCR: Vifo vya wahajiri katika Bahari ya Mediterania vimepungua
Jan 03, 2019 11:42Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limesema wahajiri wapatao 2,262 walifariki dunia katika Bahari ya Mediterania mwaka uliomalizika wa 2018, na kwamba idadi ya wahajiri wanaokufa maji katika safari hizo hatarishi imepungua kwa zaidi ya asilimia 25.
-
AU yazikosoa nchi za Ulaya zilizokataa kusaini Mkataba wa Wahajiri
Dec 18, 2018 23:21Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amezikosoa vikali nchi kadhaa za Ulaya zilizokataa kusaini Mkataba wa Kimataifa wa Wahajiri.
-
UN yataka kuzidishwa misaada kwa wahajiri
Dec 08, 2018 04:46Kamisheni Kuu ya Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa imeeleza wasiwasi wake mkubwa kuhusu hatua ya kusitishwa operesheni ya uokoaji ya meli ya Aquarius na kutoa wito wa kuzidishwa misaada ya kuokoa wahajiri katika Bahari ya Mediterania.
-
Marekani imewatenganisha makumi ya watoto wa wahajiri na familia zao
Dec 06, 2018 11:20Shirika la habari la Associated Press limevujisha data za serikali ya Washington zinazoonesha kuwa, Marekani imewatenganisha makumi ya watoto wa wahajiri na familia zao katika mpaka wa nchi hiyo na Mexico ndani ya miezi michache iliyopita.
-
Kiu na njaa yaua wahajiri 15 ndani ya boti, pwani ya Libya
Dec 04, 2018 11:10Maiti 15 za wahajiri zimepatikana zikiwa ndani ya boti katika pwani ya Libya, katika bahari ya Mediterania.
-
Miili ya wahajiri 15 yapatikana ndani ya boti katika bahari ya Mediterania
Nov 25, 2018 04:45Maiti za wahajiri 15 wa Kiafrika zimepatikana na jeshi la majini la Morocco, zikiwa ndani ya boti iliyokuwa ikielea katika bahari ya Mediterania.
-
Nduli wa mauaji ya Waislamu CAR apandishwa kizimbani ICC
Nov 23, 2018 23:16Alfred Yakatom, ambaye wakati fulani alijulikana kwa jina la Rambo kutokana na kufanya mauaji makubwa dhidi ya Waislamu huko Jamhuri ya Afrika ya Kati, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC akikabiliwa na mashtaka 14 ya jinai za kivita na jinai dhidi ya ubinadamu.