-
Wahajiri Milioni 2.5 walisafrishwa kimagendo mwaka 2016
Jun 17, 2018 07:42Wahajiri wasiopungua 2.5 walisafirishwa kimagendo mwaka 2016 ambapo wafanya magendo ya binadamu waliohusika walipata faida ya dola bilioni saba za Kimarekani.
-
UN yawawekea vikwazo vigogo 6 kwa kuhusika na magendo ya binadamu Libya
Jun 08, 2018 06:53Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetangaza kuwawekea vikwazo vigogo sita wanaotuhumiwa kuhusika na biashara haramu ya magendo ya binadamu nchini Libya.
-
Wahajiri haramu 35 wafariki baada ya boti yao kuzama baharini Tunisia
Jun 03, 2018 14:58Wahajiri 35 haramu wamepoteza maisha baada boti yao kuzama baharini nchini Tunisia huku wengine 67 wakiokolewa katika oparesheni ya gadi ya pwani ya nchi hiyo.
-
Waafrika wengi hutembelea zaidi bara hilo kuliko kutoka nje yake – Ripoti
Jun 02, 2018 04:10Uchunguzi uliofanywa na wataalamu wa kimataifa kuhusu faida za wahamiaji kwa nchi wanazotembelea na wanazotoka unaonesha kuwa, asilimia kubwa ya Waafrika wanapenda kutembelea nchi za bara hilo kuliko kutoka nje ya Afrika.
-
UN: Wafanya magendo ya binadamu waua wahajiri 12 Libya
Jun 01, 2018 13:53Umoja wa Mataifa umesema wahajiri 12 wameuawa kwa kupigwa risasi na wafanya magendo ya binadamu, walipokuwa wakijirabu kukimbia kambini nchini Libya.
-
Wahajiri 1,500 waokolewa katika bahari ya Mediterranean
May 26, 2018 07:53Takriban wahajiri 1,500 wamenusuriwa wakiwa katika safari hatarishi katika bahari ya Mediterranean, kwenye operesheni zilizofanyika siku ya Alkhamisi na jana Ijumaa.
-
Saudia kuwatimua wahajiri laki tano raia wa Ethiopia
May 20, 2018 07:29Saudi Arabia imekubali ombi la Ethiopia la kuwaachia huru wahajiri wapatao elfu moja raia wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika, lakini imesisitiza kuwa itawafukuza nchini humo malaki ya wahajiri wengine wa nchi hiyo ya Kiafrika.
-
Wahajiri wa Nigeria waishtaki Italia kwa kukanyaga haki zao
May 09, 2018 02:58Kundi la wahajiri raia wa Nigeria ambao ni manusura wa ajali za boti zilizoshuhudiwa mwaka jana wameifungulia mashitaka serikali ya Italia kwa kukiuka haki zao za binadamu.
-
Ripoti: Miamala ya serikali ya Trump kwa wahajiri, ni ya shari, kidhalimu na isiyo ya kibinaadamu
May 01, 2018 14:07Gazeti la Knoxville Daily la nchini Marekani limekosoa miamala ya serikali ya nchi hiyo kuwahusu wahajiri na kuweka wazi kwamba miamala hiyo ni ya shari, kidhalimu na isiyo ya kibinaadamu.
-
Ripoti: Wahajiri wa Kiafrika walioko US wamesoma kuliko Wamarekani wenyewe
Apr 25, 2018 02:31Utafiti uliofanywa na Kituo cha Utafiti cha Pew umeonyesha kuwa, kuna mwanya mkubwa wa kiwango cha elimu kati ya wahajiri wa Kiafrika wanaoishi Marekani na raia wa asili wa nchi hiyo.