-
Wapinzani waendelea kulalamikia matokeo ya uchaguzi Zimbabwe
Aug 09, 2018 07:55Wapinzani nchini Zimbabwe wamendelea kufanya maandamano wakilalamikia matokeo ya uchaguzi wa Rais wa hivi karibuni yaliyompa ushindi Emmerson Mnangagwa wa chama tawala cha ZANU-PF.
-
Wafuasi 28 wa upinzani Zimbabwe washtakiwa kwa kuzusha vurugu baada ya uchaguzi
Aug 05, 2018 08:15Wafuasi wasiopungua 28 wa mrengo wa upinzani nchini Zimbabwe wamepelekwa mahakamani wakikabiliwa na mashtaka ya kuzusha vurugu na machafuko baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi mkuu.
-
Rais mpya wa Zimbabwe na changamoto anazokabiliana nazo
Aug 05, 2018 02:32Emmerson Mnangagwa amechaguliwa kuwa rais wa Zimbabwe katika uchaguzi wa kwanza ambao haukumuhusisha rais wa kwanza wa nchi hiyo Robert Mugabe aliyetawala nchi hiyo kwa muda wa miaka 37. Baada ya kutangazwa matokeo rasmi ya uchaguzi huo wa Jumatatu nchi hiyo imetumbukia katika ghasia za kisiasa huku wapinzani wakidai kuwepo wizi wa kura.
-
Upinzani, fujo na machafuko yaendelea baada ya uchaguzi nchini Zimbabwe.
Aug 04, 2018 15:51Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe ameyakataa matokeo ya uchaguzi wa rais akisema ni ya "uongo".
-
Rais wa Zimbabwe asisitiza udharura wa kudumisha umoja kufuatia ghasia
Aug 04, 2018 08:13Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe ametoa wito kwa wananchi kudumisha umoja kufuatia ghasia zilizoibuka baada ya tume ya uchaguzi kumtangaza mshindi katika uchaguzi uliofanyika wiki hii.
-
Rais Emmerson Mnangagwa atangazwa mshindi wa uchaguzi wa rais Zimbabwe
Aug 03, 2018 04:25Tume ya Uchaguzi nchini Zimbabwe, imemtangaza asubuhi ya leo Rais wa sasa Emmerson Mnangagwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliofanyika siku ya Jumatatu iliyopita.
-
Jeshi la Zimbabwe laamuru kufungwa maduka yote Harare, matokeo ya uchaguzi karibuni
Aug 02, 2018 14:05Jeshi la Zimbabwe limeamuru kufungwa maduka yote na kuwataka watu kuondoka katika maeneo ya katikati mwa mji mkuu wa nchi hiyo, Harare, siku moja baada ya watu watatu kuuawa kwa kupigwa risasi na askari usalama waliotumwa kuzima maandamano ya watu waliodai kuwa matokeo ya uchaguzi wa rais yamechakachuliwa.
-
Watatu wauawa Zimbabwe, askari usalama wapambana na wapinzani wanaopinga matokeo ya uchaguzi
Aug 02, 2018 08:07Polisi ya Zimbabwe imesema watu watatu waliuawa jana wakati askari walipokuwa wakiwatawanya wafuasi wa upinzani waliokuwa wakirembea mawe huku wakikituhumu chama tawala cha Zanu-PF kuwa kinajaribu kuchakachua matokeo ya uchaguzi uliofanyika siku ya Jumatatu.
-
Askari wapambana na wafuasi wa upinzani Zimbabwe huku ZANU-PF ikipata ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa bunge
Aug 01, 2018 16:37Milio ya risasi ya bunduki za otomatiki imesikika katika mitaa ya mji mkuu wa Zimbabwe, Harare leo wakati askari walipoingilia kati kuwatawanya waandamanaji waliopambana na polisi baada ya kiongozi mkuu wa upinzani kukituhumu chama tawala cha Zanu-PF kuwa kinajaribu kuyachakachua matokeo ya uchaguzi.
-
Mnangagwa na Chamisa wasema wana matumaini ya kushinda uchaguzi wa Rais Zimbabwe
Jul 31, 2018 15:58Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe na mgombea wa chama cha MDC, Mchungaji Nelson Chamisa wamesema wote kuwa wana matumaini ya kushinda katika uchaguzi wa rais uliofanyika jana nchini humo.