Serikali ya Jordan yaipiga marufuku harakati kongwe ya Kiislamu ya Ikhwanul-Muslimin
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jordan ametangaza kuwa utawala huo wa kifalme umeipiga marufuku harakati ya Kiislamu ya Ikhwanul-Muslimin na kuielezea "itikadi" yake inayohubiri kuwa sasa ni 'haramu' kisheria nchini humo.
Harakati hiyo kongwe ya Kiislamu imekuwa kwa muda mrefu ikiendesha harakati zake kwa njia za amani zinazoshajiisha kushiriki katika siasa za kidemokrasia, lakini inachukiza mbele ya tawala nyingi za kiimla katika Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini.
Katika miaka ya karibuni, tawi la Ikhwanul-Muslimin nchini Jordan limekuwa halisikiki sana, ingawa wanachama wake na watu wenye mfungamano nalo wamekuwa wakilaani vikali vita vya kinyama na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ghaza na kuwatolea wito Waarabu wawaunge mkono na kuwasaidia wananchi hao wanaodhulumiwa.
Utawala wa kifalme wa Jordan ni miongoni mwa nchi chache za Kiarabu zenye uhusiano rasmi wa kidiplomasia na utawala haramu wa Israel.../