Maafisa wawili wa usalama wa Saudia wauawa mjini Dammam
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i18133-maafisa_wawili_wa_usalama_wa_saudia_wauawa_mjini_dammam
Watu wasiojulikana wamewapiga risasi na kuwaua maafisa wawili wa usalama katika mji wa Dammam mashariki mwa Saudi Arabia.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Oct 25, 2016 12:52 UTC
  • Maafisa wawili wa usalama wa Saudia wauawa mjini Dammam

Watu wasiojulikana wamewapiga risasi na kuwaua maafisa wawili wa usalama katika mji wa Dammam mashariki mwa Saudi Arabia.

Taarifa zinasema washambuliaji hao waliwafyatulia risasi maafisa hao wa usalama leo Jumanne wakati wakitoka kazini wakiwa ndani ya gari binafsi.

Saudi Arabia imekuwa ikishuhudia visa vya ufyatuaji risasi na mashambulizi ya mabomu tokea vikosi vya usalama vianze kuwalenga Waislamu wa madhehebu ya Shia katika kipindi cha mwaka mmoja sasa.

Mwezi Septemba, maafisa wawili wa polisi walipigwa risasi na kuuawa Dammam, mji mkuu wa mkoa wa Mashariki ambao wakaazi wake wengi ni Waislamu wa madhehebu ya Shia  wanaokandamizwa na utawala wa Saudia. Aidha kumekuwepo na hujuma kadhaa dhidi ya misikiti ya Waislamu wa madhehebu ya Shia katika eneo hilo.

Magaidi wa ISIS

Serikali ya Saudia inalaumu magaidi wa kitakfiri wa ISIS au Daesh kuwa ndio wanaotekeleza hujuma hizo. Ikumbukwe kuwa magaidi wa ISIS wanafuata itikadi ya Kiwahabi ambayo ni itikadi rasmi ya Saudi Arabia.