Askari na mamluki wa Saudia wazidi kuangamizwa na vikosi vya Yemen
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i22045-askari_na_mamluki_wa_saudia_wazidi_kuangamizwa_na_vikosi_vya_yemen
Mamluki wasiopungua 16 wa Saudi Arabia huko nchini Yemen wameangamizwa kufuatia operesheni ya kijeshi ya jeshi la Yemen likisaidiwa na vikosi vya kujitolea vya wananchi.
(last modified 2026-02-21T22:51:18+00:00 )
Dec 24, 2016 04:27 UTC
  • Askari na mamluki wa Saudia wazidi kuangamizwa na vikosi vya Yemen

Mamluki wasiopungua 16 wa Saudi Arabia huko nchini Yemen wameangamizwa kufuatia operesheni ya kijeshi ya jeshi la Yemen likisaidiwa na vikosi vya kujitolea vya wananchi.

Kanali ya televisheni ya al-Masira ya Yemen imeripoti kuwa, askari watatu wa Saudia wameuawa kwa kufyatuliwa risasi na vikosi vya Yemen katika eneo la al-Mazraq  mkoa wa Jizan na eneo la milima la Tabat al-Hamrah, kusini mashariki mwa Saudia, huku mamluki zaidi ya 10 wa utawala huo wa kifalme wakiuawa katika maeneo mengine ya Yemen.

Aidha mamluki wengine watatu wa Saudia wameuawa katika shambulizi la roketi la vikosi vya Yemen, katika wilaya ya al-Ghayl, kaskazini mwa mkoa wa Jawf. 

Hujuma ya anga ya Saudia nchini Yemen

Haya yanajiri siku tatu baada ya mamluki wasiopungua 97 wa Saudi Arabia huko nchini Yemen kuangamizwa kufuatia operesheni ya kijeshi ya kamati za wananchi huku wengine 50 wakijeruhiwa.

Majeshi ya Saudi Arabia na washirika wake kama Marekani, Israel na nchi kadhaa za Kiarabu, yalianza kulishambulia taifa la Yemen mwezi Machi mwaka jana kwa kisingizio cha kumrejesha madarakani rais aliyetoroka nchi na kukimbilia Saudia, Abd Rabbuh Mansur Hadi.  

Mashambulio hayo ya kinyama ya Saudia hadi sasa yameshaua zaidi ya Wayemeni elfu kumi, kujeruhi mamia ya maelfu ya wengine au kuwaacha bila makazi mbali na kuteketeza asilimia 80 ya taasisi za miundombinu na za utoaji huduma na tiba za nchi hiyo masikini ya Kiarabu.

Kimya cha UN mbele ya jinai za Saudia nchini Yemen