-
Sheikh Issa Qassim: Uchaguzi wa Bahrain ni wa kidhulma na siyo wa kiadilifu
Oct 20, 2022 09:14Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Bahrain amesema kuwa, uchaguzi wa Bahrain ni wa kidhulma na siyo wa kiadilifu.
-
MOSSAD imeua maafisa wake sita wa intelijensia kwa tuhuma za kuwa na uhusiano na Iran
Oct 20, 2022 04:41Utawala haramu wa Kizayuni wa Israel umewaua maafisa wake sita muhimu kufuatia kufeli operesheni ya shirika lake la ujasusi Mossad ya kufanya hujuma na uharibifu kwenye kituo kimoja cha viwanda mkoani Esfahan nchini Iran.
-
Afungwa jela miezi 13 kwa kuandika sentensi moja ya kuunga mkono Muqawama wa Palestina
Oct 20, 2022 04:01Mahakama ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel imemhukumu Mpalestina mmoja anayeishi katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu kifungo cha miezi 13 jela kwa kuandika mtandaoni sentensi moja ya kuunga mkono muqawama wa Palestina.
-
Ujumbe wa HAMAS waonana na Rais wa Syria mara ya kwanza baada ya miaka 10
Oct 19, 2022 21:15Duru za Syria zimetangaza habari ya kukutana ujumbe mmoja wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS na Rais Bashar al Assad wa nchi hiyo ikiwa ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 10 iliyopita.
-
UN: 2022, mwaka wa mauaji zaidi katika ardhi za Palestina katika miaka 16 iliyopita
Oct 19, 2022 07:02Mratibu wa Misaada ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika Maeneo Yanayokaliwa kwa Mabavu ametangaza katika ripoti yake kwamba mwaka huu wa 2022 ulikuwa mwaka wa umwagaji damu zaidi katika ardhi za Palestina katika kipindi cha miaka 16 iliyopita.
-
Qatar: Hatutoi gesi ya wateja wa Asia kwenda Ulaya
Oct 19, 2022 04:40Waziri wa Masuala ya Nishati wa Qatar ametangaza kuwa haitazamiwi katika msimu ujao wa baridi kali shehena ya gesi iliyopangwa kwenda Asia kuelekea Ulaya.
-
Utawala wa Kizayuni wakasirishwa na Australia kubadilisha msimamo wake kuhusu Baitul Muqaddas
Oct 19, 2022 02:29Viongozi wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel wamesema wamekasirishwa na hatua ya serikali mpya ya Australia ya kufuta uamuzi wa serikali iliyopita wa kuitambua Baitul Muqaddas (Jerusalem) kuwa mji mkuu wa utawala huo ghasibu.
-
Serikali ya India iliidhinisha kuachiwa huru waliombaka mwanamke Muislamu na kuwaua watu wa familia yake
Oct 18, 2022 23:07Serikali ya Waziri Mkuu wa India Narendra Modi iliidhinisha kuachiliwa huru mnamo mwezi Agosti wanaume 11 waliopatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kumbaka mwanamke Mwislamu na kuwaua watu wa familia yake wakati wa ghasia za kidini zilizotokea katika jimbo la Gujarat mwaka 2002. Hayo ni kulingana na hati za mahakama.
-
Sheikh Naim Qassim: Rais mpya anapasa kuunga mkono haki za Walebanoni wote
Oct 18, 2022 07:04Naibu Katibu Mku wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa rais mpya wa nchi hiyo anapasa kuwa mtetezi wa haki za Walebanoni wote.
-
Sheikh Naim Qassim: Muqawama una taathira kubwa katika kudhamini haki ya baharini ya Lebanon
Oct 17, 2022 01:47Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, kuwepo muqawama kumekuwa na tatahira kuu katia kudhamini haki za mafuta, gesi na mali nyingine za baharini za Lebanon.