-
Matamshi ya Huckabee yalaaniwa vikali katika Ulimwengu wa Kiislamu, yaitwa ya 'kipuuzi' na 'kichochezi'
Feb 22, 2026 06:50Matamshi ya balozi wa Marekani katika utawala wa kizayuni wa Israel Mike Huckabee kwamba utawala huo ghasibu una haki ya kupanua eneo lake kwa kupora eneo kubwa la Mashariki ya Kati la nchi kadhaa za Kiarabu na Kiislamu za eneo hilo yamekosolewa na kulaaniwa vikali na nchi hizo, Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu, OIC, Jumuiya ya Waarabu na makundi ya ukombozi wa Palestina.
-
Wazayuni washadidisha mashambulizi Ukingo wa Magharibi katika mwezi wa Ramadhani
Feb 22, 2026 06:48Sambamba na kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani, jeshi la utawala wa Kizayuni limeshadidisha mashambulizi yake katika maeneo mbalimbali ya Ukingo wa Magharibi huko Palestina.
-
Ansarullah: Kujizatiti upya kijeshi maadui katika eneo ni ishara kwamba Muqawama ungali hai
Feb 21, 2026 11:08Mjumbe mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Yemen ya Ansarullah ametoa taarifa akieleza kwamba kuzungumziwa duru mpya ya vita vinavyotaka kuanzishwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Muqawama ni sawa na adui kukiri kwamba alishindwa katika vita vilivyopita.
-
Licha ya vizuizi vikali vya Israel, Wapalestina laki moja wasali I'sha na Tarawehe Masjidul-Aqsa
Feb 21, 2026 11:07Licha ya vizuizi vikali vilivyowekwa na utawala wa Kizayuni wa Israel vya kuingia katika Msikiti wa Al-Aqsa, makumi ya maelfu ya Wapalestina jana usiku walihudhuria katika msikiti huo mtukufu kusali Sala za I'sha na Tarawehe wakati huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Mtazamo wa Moscow kuhusu maneva ya pamoja ya baharini kati ya Iran, Russia na China
Feb 21, 2026 09:11Moscow imetangaza kuwa mazoezi ya pamoja ya majini kati ya majeshi ya Iran, Russia na China yatafanyika katika Lango -Bahari la Hormuz.
-
Balozi wa Marekani: Ni sawa ikiwa Israel itanyakua ardhi kote Asia Magharibi
Feb 21, 2026 07:35Balozi wa Marekani katika utawala Israel amesema itakuwa “sawa tu” iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utapanua mipaka yake kote katika Asia Magharibi chini ya mpango wa “Israeli Kubwa.”
-
Ripota wa UN kuhusu Palestina asema, licha ya kuandamwa hatasalimu amri, hatajiuzulu
Feb 21, 2026 02:36Francesca Albanese, ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa wa maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu, amesema hatajiuzulu wadhifa wake huo licha ya mashinikizo yanayotolewa dhidi yake na serikali za nchi kadhaa za Ulaya kutokana na matamshi yanayodaiwa kuwa ametoa dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Israel yawazuia Wapalestina kuswali Ijumaa ya kwanza ya Ramadhani al-Aqsa
Feb 20, 2026 13:07Utawala wa Kizayuni wa Israel umewawekea vizuizi vikali Wapalestina kuingia katika Msikiti wa al-Aqsa katika mji wa Quds unaokaliwa kwa mabavu, kwa ajili ya Swala ya Ijumaa ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, huku mamia ya watu wakipanga foleni kwenye kizuizi cha Qalandiya karibu na Ramallah wakitarajia kuingia.
-
Hamas yalaani mkutano wa 'Bodi ya Amani' ya Trump
Feb 20, 2026 09:48Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imelaani vikali kufanyika mkutano wa kile kinachoitwa 'Bodi ya Amani ya Gaza' huko nchini Marekani.
-
Zaidi ya Wapalestina na Waarabu 9,300 wanashikiliwa mateka katika magereza ya Israel
Feb 20, 2026 07:11Klabu ya Wafungwa wa Palestina imetangaza kuwa, zaidi ya mateka na wafungwa 9,300 wa Palestina na Kiarabu wanashikiliwa katika magereza ya utawala ghasibu wa Israel na wamekuwa wakikabiliwa na sera za mateso, njaa, na mauaji ya taratibu tangu kuanza "mauaji ya kimbari ya Israel" mnamo Oktoba 7, 2023.