Mahakama ya Korea Kusini yatoa kibali cha kukamatwa kwa Yoon
-
Yoon Suk-yeol
Mahakama ya Korea Kusini imetoa waranti ya kukamatwa Rais wa nchi hiyo anayeandamwa na Bunge, Yoon Suk-yeol kutokana uamuzi wake wa kutangaza sheria ya kijeshi mnamo Desemba 3.
Mahakama ya Wilaya ya Seoul Magharibi mapema leo Jumanne imedhinisha hati hiyo kufuatia ombi la Makao Makuu ya Upelelezi wa Pamoja, ambayo inamchunguza kiongozi huyo wa Korea Kusini kutokana na kusababisha machafuko na matumizi mabaya ya madaraka.
Hatua hiyo ni mara ya kwanza kwa mamlaka kutaka kumweka kizuizini Rais aliyeko madarakani nchini Korea Kusini.
Kibali cha sasa cha kukamatwa kinaweza kutumika hadi Januari 6, na mara amri hiyo itakapotekelezwa, Yoon atazuiliwa katika gereza jijini Seoul.
Yoon amekataa wito wa wapelelezi kuhojiwa mara tatu tangu kutangazwa kwa sheria ya kijeshi Desemba 3.
Yoon anakabiliwa na uwezekano wa kufungwa jela maisha, au hata hukumu ya kifo, kutokana na utangazaji wake wa sheria ya kijeshi mnamo Desemba 3, ambao ililiitumbukiza taifa hilo la Asia Mashariki katika mgogoro mkubwa zaidi wa kisiasa katika miongo kadhaa.