Russia yalaani 'uharamia' wa Marekani wa kukamata meli yake ya mafuta
Moscow imelaani vikali kitendo cha Marekani cha kukamata meli ya mafuta yenye bendera ya Russia katika Bahari ya Atlantic, na kuitaja hatua hiyo kama ukiukaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa Kuhusu Sheria ya Bahari.
Kamandi ya Jeshi la Marekani katika nchi za Umoja wa Ulaya ilitangaza kukamata meli ya Marinera, ambayo awali ilijulikana kama 'Bella 1', inayohusishwa na mafuta ya Venezuela, jana Jumatano kwa madai ya "kukiuka vikwazo vya Marekani."
Wizara ya Uchukuzi ya Russia imethibitisha kukamatwa kwa meli hiyo, ikisema mawasiliano na meli hiyo yalipotea baada ya vikosi vya wanamaji vya Marekani kukipanda katika maji ya kimataifa.
"Kwa mujibu wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Sheria ya Bahari ya 1982, uhuru wa safari za baharini unatumika katika maji ya kimataifa, na hakuna serikali iliyo na haki ya kutumia nguvu dhidi ya vyombo vilivyosajiliwa kihalali katika mamlaka ya mataifa mengine," imesema taarifa ya wizara hiyo.
Wakati huo huo, Uingereza imetangaza kuwa ilitoa "msaada uliowezesha" jeshi la Marekani kukamata meli hiyo ya mafuta yenye bendera ya Russia ya Marinera. Hayo ni kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya Uingereza imesema.
Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza mwezi Disemba "vizuizi kamili" vya meli za mafuta zilizoidhinishwa zinazoingia na kutoka Venezuela. Baada ya kutekwa nyara kwa Maduro, Trump alisema Venezuela "itakabidhi" hadi mapipa milioni 50 ya mafuta kwa Marekani.