Kansela wa Ujerumani asisitiza kuhusu nafasi ya jiostratejiki ya Russia kimataifa
https://parstoday.ir/sw/news/world-i63136-kansela_wa_ujerumani_asisitiza_kuhusu_nafasi_ya_jiostratejiki_ya_russia_kimataifa
Kansela wa Ujerumani amesema kuwa Russia ni nchi iliyo na nafasi ya jio-stratejiki na ametaka mazungumzo yafanyike kati ya Berlin na Moscow.
(last modified 2026-04-28T05:09:17+00:00 )
Aug 31, 2020 03:13 UTC
  • Kansela wa Ujerumani asisitiza kuhusu nafasi  ya jiostratejiki ya Russia kimataifa

Kansela wa Ujerumani amesema kuwa Russia ni nchi iliyo na nafasi ya jio-stratejiki na ametaka mazungumzo yafanyike kati ya Berlin na Moscow.

Bi Angela Merkel ameeleza kuwa Russia ikiwa nchi yenye nafasi ya jiostratejiki ina mchango muhimu katika kadhia mbalimbali za kimataifa kama zile za Syria na Libya na kuongeza kuwa: kuna udharura wa kushirikiana zaidi Berlin na Moscow katika uwanja huo kuliko ilivyokuwa huko nyuma. 

Kansela wa Ujerumani amesema kuwa, Russia ni nchi kubwa yenye historia kongwe na utamaduni tajiri na kusistiza kuwa kuimarisha uhusiano na Moscow ni katika vipaumbele vya ajenda  za siasa zake za nje. 

Nchi kubwa ya Russia yenye nafasi muhimu katika masuala mbalimbali kimataifa 

Kukiri Kansela wa Ujerumani ambayo inahesabiwa kuwa nchi muhimu zaidi katika Umoja wa Ulaya na yenye nafasi nyeti ndani ya umoja huo na katika Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi (Nato)  kuhusu nafasi muhimu ya Russia katika kadhia za kimataifa kunaashiria kubadilika misimamo ya kambi ya Magharibi mkabala na taswira na nafasi iliyonayo sasa Russia duniani.