-
Ushiriki wa Wamarekani kwenye mazishi ya Ayatullah Khamenei waibua hasira huko Washington
Jul 12, 2026 04:11Mazishi ya aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Shahidi Ayatullah Ali Khamenei, hayakuwa tukio la Iran pekee; bali pia uwepo mkubwa wa watu wenye ushawishi na wanablogu wa kigeni katika shughuli hiyo, wakiwemo Wamarekani ambao wamesema walikwenda Iran kuonyesha mshikamano wao na kutetea simulizi ya nchi hiyo mbele ya Marekani na Israel, umezusha hasira kubwa katika duru za Magharibi.
-
Russia na China zapinga mashinikizo ya Magharibi dhidi ya Iran katika Baraza la Usalama
Jul 11, 2026 11:31Russia na China zimepinga vikali kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) kilichochochewa na nchi za Magharibi kuhusu Iran siku ya Ijumaa, zikisisitiza kuwa Azimio namba 2231 lilifika ukingano mnamo Oktoba 2025, na hivyo Baraza hilo halina tena mamlaka ya kisheria kujadili suala la nyuklia la Tehran.
-
Malalamiko rasmi dhidi ya Infantino wa FIFA kuhusu uhusiano Wake na Trump
Jul 11, 2026 04:32Shirika moja la kutetea haki za binadamu na usimamizi wa michezo limetangaza mpango wake wa kuwasilisha malalamiko dhidi ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), Gianni Infantino, kwa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC). Shirika hilo linamtuhumu Infantino kwa kukiuka mara kwa mara sheria za kutofungamana na upande wowote katika masuala ya kisiasa, kupitia uungaji mkono wake wa wazi na uhusiano wa karibu na Rais wa Marekani, Donald Trump.
-
Mauaji ya kimbari, ubaguzi wa rangi, na ukoloni... Je, Kanisa la Uingereza limeipa mgongo Israel?
Jul 11, 2026 03:03Gazeti la Times la London limeripoti kwamba Rabi Mkuu wa Mayahudi wa Uingereza, Sir Ephraim Mirvis, amelitaka Kanisa la Uingereza kukataa kujadili ripoti inayoelezea vita vya Israel huko Gaza kuwa ni "mauaji ya kimbari," akidai kwamba kupitishwa hati hiyo kunaweza kuharibu uhusiano kati ya Wayahudi na Wakristo uliojengwa kwa miongo kadhaa.
-
Iran: Hatua za Marekani ni mfano wa wazi wa uhalifu mkubwa wa kivita
Jul 11, 2026 02:41Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema, mashambulizi yaliyofanywa na jeshi la Marekani dhidi ya maeneo kadhaa katika mikoa ya pwani ya kusini mwa nchi pamoja na madaraja mawili yaliyopo katika mikoa ya mashariki kwenye njia ya reli inayoelekea mji mtakatifu wa Mashhad, yanajumuisha uhalifu mkubwa wa kivita.
-
Saratani inaua 26,000 kwa siku, WHO yafichua pengo la maisha kati ya matajiri na maskini
Jul 09, 2026 10:42Ripoti mpya ya Shirika la Afya Duniani (WHO) imeonya kwamba saratani inaweka mzigo mkubwa wa kibinadamu na kiuchumi kwa jamii duniani kote, ikichukua uhai wa zaidi ya watu 26,000 kila siku na kudhihirisha ukosefu mkubwa wa usawa katika viwango vya maisha kati ya nchi tajiri na maskini.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa zamani wa Austria: Iran sasa ni dola kubwa lenye ushawishi
Jul 07, 2026 03:25Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Austria amesema, akiashiria nafasi ya ustaarabu wa maelfu ya miaka wa Iran katika historia ya dunia, kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa sasa imegeuka kuwa moja ya mataifa makubwa yenye ushawishi katika ngazi ya kimataifa.
-
Idadi kubwa ya wapiga kura wa Marekani wasema vita vya Trump dhidi ya Iran havina tija
Jul 06, 2026 10:24Idadi kubwa ya wapiga kura nchini Marekani wanaamini kuwa vita vya Donald Trump dhidi ya Iran havijazalisha tija inayostahili gharama zilizotumika. Kulingana na utafiti mpya wa gazeti la Financial Times, hali hiyo inaashiria jinsi mzozo huo unavyozidi kudhoofisha uungaji mkono kwa mtawala huyo kuelekea uchaguzi wa katikati wa muhula mwezi Novemba.
-
Ubelgiji yalaani FIFA kuhusu kuruhusiwa kwa mshambuliaji wa Marekani licha ya kadi nyekundu
Jul 06, 2026 07:32Shirikisho la Soka la Ubelgiji limeonyesha ghadhabu kubwa kufuatia uamuzi wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, kumruhusu mshambuliaji wa Marekani, Folarin Balogun, kushiriki katika mechi muhimu ya hatua ya 16 bora dhidi ya Ubelgiji siku ya Jumatatu, licha ya mchezaji huyo kuonyeshwa kadi nyekundu katika mzunguko uliopita.
-
Makundi ya Ulaya yanayopinga ubeberu yawasili Iran kwa mazishi ya Kiongozi Shahidi
Jul 03, 2026 03:53Misafara ya wanaharakati wanaopinga ubeberu, wasomi, waandishi wa habari na wawakilishi wa vituo vya Kiislamu kutoka kote barani Ulaya inaendelea kuwasili Tehran kushiriki katika mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliyeuawa shahidi katika shambulizi la kushtukiza la Marekani na Israel.