-
Mawakili wa Marekani, Palestina na Jordan kupinga uamuzi wa Trump kuhusu Quds
Mar 13, 2018 15:54Wanasheria na mawakili kadhaa wa Marekani, Palestina na Jordan wametangaza kuwa wako tayari kufungua mashtaka mahakamani dhidi ya uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani na Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu wa kuitambua Quds tukufu (Jerusalem) kuwa mji mkuu wa utawala haramu wa Israel na kutaka kuhamishia ubalozi wa Marekani katika mji huo.
-
Uamuzi wa Trump kuhusu Quds waendelea kupingwa
Mar 09, 2018 16:04Wimbi jipya la upinzani dhidi ya maamuzi ya viongozi wa Marekani wanaotaka kutambuliwa Quds (Jerusalem) kama mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, limechukua mkondo wake.
-
Uzembe wa nchi za Kiarabu umeongeza uadui Marekani dhidi ya Quds Tukufu
Mar 09, 2018 06:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina, Riyadh Al-Maliki amesema, uzembe na upuuzaji wa nchi za Kiarabu kuhusu kadhia ya Palestina katika kipindi cha miongo kadhaa iliyopita ndicho chanzo cha kuongezeka uadui na jeuri za Marekani dhidi ya Quds Tukufu.
-
Rais wa Ufaransa ampinga Trump, ataka Beitul-Muqaddas itambuliwe kuwa mji mkuu wa Palestina
Mar 08, 2018 04:33Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amesema kuwa, umewadia wakati sasa wa Beitul-Muqaddas kutambuliwa kuwa mji mkuu wa Palestina.
-
Wakristo Quds: Tutaendelea kuwashinda Wazayuni waliozivamia ardhi za Palestina
Mar 01, 2018 04:38Wakristo wa mji wa Quds wamefurahishwa na hatua ya kufunguliwa upya kanisa kuu la 'Al-Qiyamah' baada ya kufungwa kwa siku kadhaa na utawala haramu wa Israel na kuitaja hatua hiyo kuwa ni katika safari ya kuelekea ushindi kamili dhidi ya Wazayuni hao wanaokalia kwa mabavu ardhi za Palestina.
-
Sheikh wa al-Aqsa aonya kuhusu huhamishiwa Quds ubalozi wa US
Feb 28, 2018 07:58Mhubiri mtajika wa Msikiti wa al-Aqsa, Sheikh Ikrima Sabri ametahadharisha kuhusu azma ya Marekani ya kuuhamishia ubalozi wake mjini Quds Tukufu kutoka Tel Aviv na kuitaja hatua hiyo kama ya kichokozi na kichochezi.
-
Hamas yatoa wito wa maandamano ya kupinga kuhamishiwa Quds ubalozi wa Marekani
Feb 26, 2018 02:41Harakati ya Mapambanao ya Kiislamu ya Palestina Hamas imetoa mwito wa kufanyika maandamano ya kupinga nia ya Marekani ya kutaka kuuhamishia Quds ubalozi wake ulioko Tel Aviv, karibuni hivi.
-
Jumuiya ya Nchi za Kiarabu yalaani tangazo la kuhamishia ubalozi wa Marekani Quds Tukufu
Feb 25, 2018 07:23Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imelaani vikali hatua ya Marekani kutangaza kuwa itahamisha ubalozi wake kutoka Tel Aviv hadi Quds Tukufu (Jerusalem).
-
Kigogo wa makasino kugharamia kuhamishiwa ubalozi wa Marekani Baitul-Muqaddas
Feb 25, 2018 02:49Sheldon Adelson, bilionea wa Kiyahudi ambaye ni muungaji mkono mkubwa wa utawala ghasibu wa Israel ametangaza kuwa, atatoa gharama za kuhamishiwa ubalozi wa Marekani huko Baitul-Muqaddas.
-
Marekani kuuhamishia Quds (Jerusalem) ubalozi wake wa Tel Aviv mwezi Mei mwaka huu
Feb 24, 2018 03:58Licha ya upinzani mkubwa ulioanzia eneo la Mashariki ya Kati na ulimwengu kwa jumla, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imetangaza kuwa mnamo mwezi Mei mwaka huu ubalozi wa nchi hiyo ulioko Tel Aviv utahamishiwa Baitul Muqaddas inayokaliwa kwa mabavu.