-
Maambukizi ya aina mpya ya spishi ya Omicron yachachamaa Afrika Kusini
Feb 05, 2022 01:08Afrika Kusini imeshuhudia ongezeko la maambukizi ya aina mpya ya spishi ya kirusi cha Corona cha Omicron, iliyopewa jina la kitaalamu la BA.2.
-
Aliyechoma moto Bunge la Afrika Kusini kuhukumiwa Februari 4
Jan 31, 2022 00:34Zandile Mafe atajua hatima yake siku chache zijazo baada ya mahakama ya jimbo la Cape Town nchini Afrika Kusini kueleza kuwa itatoa hukumu kuhusu mtuhumiwa huyo tarehe 4 mwezi ujao wa Februari. Zandile Mafe anakabiliwa na tuhuma za kuchoma kwa makusudi jengo la Bunge la Afrika Kusini
-
Simba waambukizwa Corona na wahudumu wa mbuga Afrika Kusini
Jan 20, 2022 00:56Wanasayansi wa Chuo Kikuu cha Pretoria nchini Afrika Kusini wamesema simba watatu na puma wawili waliopatikana na maambukizi ya virusi vya Corona waliambukizwa na wafanyakazi wa mbuga moja ya wanyamapori nchini humo.
-
Waislamu Afrika Kusini wataka kulindwa turathi za kale Cape Town
Jan 16, 2022 04:35Wanaharakati wa Kiislamu katika wilaya ya Bo-Kaap jijini Cape Town nchini Afrika Kusini wametoa mwito wa kulindwa na kuhifadhiwa turathi na athari za kale hususan za kidini katika eneo hilo ambalo aghalabu ya wakazi wake ni Waislamu.
-
Vinasaba vya askari wa Afrika Kusini wanaolinda amani DRC vyakusanywa ili kubaini baba za watoto
Jan 13, 2022 00:42Jeshi la Afrika Kusini limepeleka timu yake kwenye ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo MONUSCO, ili kuchunguza vinasaba (DNA) vya watoto na wanawake waliobakwa na walinda amani ili hatimaye kuthibitisha iwapo watuhumiwa ni walinda amani kutoka Afrika Kusini na kisha watoto hao watambue baba zao na pia kupatiwa malezi.
-
Upinzani Afrika Kusini wakituhumu chama tawala kuliteketeza kwa moto jengo la Bunge
Jan 03, 2022 08:48Mmoja wa viongozi wa vyama vya upinzani nchini Afrika kusini amekituhumu chama tawala cha Kongresi ya Taifa cha nchi hiyo (ANC) kuwa kimehusika na moto ulioteketeza kikamilifu sehemu ya jengo la Bunge la nchi hiyo.
-
Moto uliochoma Bunge Afrika Kusini, Ramaphosa atoa amri ya kufanyika uchunguzi
Jan 03, 2022 04:09Rais wa Afrika Kusini ametoa amri ya kufanyika uchunguzi wa kina na wa haraka baada ya jengo la Bunge la nchi hiyo kuteketea kikamilifu kwa moto mjini Cape Town. Jengo hilo lina umri wa miaka 138.
-
Wazimamoto Afrika Kusini wadhibiti moto uliounguza majengo ya Bunge, Cape Town
Jan 02, 2022 07:21Ripoti kutoka Afrika Kusini zinasema kuwa kikosi cha zimamoto kimefanikiwa kudhibiti kwa kiasi fulani moto mkubwa uliokuwa ukiunguza jengo la Bunge la nchi hiyo jijini Cape Town.
-
Ramaphosa: Desmond Tutu alikuwa mzalendo asiye na kifani
Dec 26, 2021 23:13Katika ujumbe wake kwenye mtandao wa Twitter, Rais wa Afrika Kusini amemtaja Askofu Mkuu Desmond Tutu, mwanaharakati wa vuguvugu la kupinga ubaguzi wa rangi nchini humo, kuwa alikuwa mzalendo wa kipekee.
-
Mahakama yamwamuru rais wa zamani wa Afrika Kusini arudi jela kumaliza kifungo chake
Dec 15, 2021 11:26Mahakama Kuu ya Afrika Kusini imemwamuru aliyekuwa rais wa nchi hiyo Jacob Zuma arudi jela baada ya kufuta uamuzi wa kumtoa kifungoni kwa sababu za kitiba.