-
Afrika Kusini yaikosoa UK kwa kusimamisha safari za ndege, kisa spishi mpya ya corona
Nov 27, 2021 01:08Afrika Kusini imeikosoa vikali serikali ya Uingereza kwa kupiga marufuku raia wa hiyo pamoja na nchi za Botswana, Namibia, Zimbabwe, Lesotho na Eswatini kuingia katika nchi hiyo ya Ulaya, kufuatia kugunduliwa spishi mpya ya corona kwa jina B.1.1.529 katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.
-
Wasiwasi mkubwa wazuka baada ya spishi mpya ya kirusi cha corona kugunduliwa nchini Afrika Kusini
Nov 26, 2021 04:34Wanasayansi wa Afrika Kusini wamesema wana wasiwasi mkubwa kutokana na spishi mpya ya kirusi cha corona iliyogunduliwa nchini humo ingawa ni katika kiwango kidogo na kwamba wanaendelea na uchunguzi ili kubaini athari kinachoweza kusababisha.
-
Ramaphosa: Afrika Kusini inakabiliwa na 'janga' la dhulma dhidi ya wanawake
Nov 23, 2021 03:57Rais wa Afrika Kusini amesema dhulma za kijinsia na ukandamizaji unaofanywa na wanaume dhidi ya wanawake ni 'janga' la pili linaloisumbua nchi hiyo kwa sasa, mbali na tandavu ya ugonjwa wa Covid-19.
-
Algeria na Afrika Kusini zapinga tena Israel kuwa mwanachama mtazamaji katika AU
Nov 16, 2021 13:21Algeria na Afrika Kusini zimetangaza tena msimamo wao wa kupinga utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kuwa mwanachama mtazamaji katika Umoja wa Afrika, AU.
-
Afrika Kusini 'yamnawa' raia wake atakayeshiriki tamasha la ulimbwende Israel
Nov 15, 2021 08:15Serikali ya Pretoria imejibari na uamuzi wa 'Bi Afrika Kusini' Lalela Mswane wa kukubali mwaliko wa kushiriki Tamasha la Ulimbwende linalotazamiwa kufanyika mwezi ujao huko Israel.
-
Balozi wa Afrika Kusini Tehran ataka Iran iondolewe vikwazo
Nov 06, 2021 04:36Balozi wa Afrika Kusini katika mji wa Tehran amesema kuondolewa vikwazo dhidi ya Iran ni kwa maslahi ya jamii ya kimataifa. Ameongeza kuwa kuondolewa vikwazo hivyo kutakuwa na manufaa kwa nchi nyingi duniani.
-
Watafiti wa Afrika Kusini wagundua fuvu la mwanadamu wa miaka laki mbili na nusu iliyopita
Nov 05, 2021 07:26Timu ya watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Witwatersrand na vyuo vikuu vingine 13 siku ya Alhamisi ya jana ilitangaza kugunduliwa kwa sehemu za fuvu la kichwa na meno ya mtoto aliyefariki dunia takriban miaka 250,000 iliyopita anayekadiriwa kuwa alikuwa na takriban miaka minne hadi sita.
-
ANC yaongoza matokeo ya awali ya uchaguzii wa serikali za mitaa Afrika Kusini
Nov 02, 2021 12:45Matokeo ya awali ya uchaguzi wa serikali za mitaa nchini Afrika Kusini uliofanyika Jumatatu ya jana yanakipatia chama tawala cha African National Congress (ANC) asilimia 46 ya kura. Matokeo hayo yametajwa kuwa ni ya zaidi ya robo ya vituo vya kupigia kura kote nchini humo.
-
Iran na Afrika Kusini zaafikiana kuimarisha ushirikiano wao
Oct 11, 2021 23:41Serikali za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Afrika Kusini zimeazimia kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa pande mbili katika nyuga za kieneo na kimataifa.
-
Upinzani nchini Afrika Kusini wataka Jacob Zuma arudishwe jela
Sep 11, 2021 03:01Upinzani nchini Afrika Kusini umewasilisha malalamiko mahakamani ukitaka rais wa zamani wa nchi hiyo Jacob Zuma arejeshwe gerezani.