-
Watoto wa Kiiraqi; wahanga wakubwa wa ugaidi
Jan 07, 2018 23:01Wizara ya Kazi na Masuala ya Jamii ya Iraq imetangaza kupitia taarifa iliyotoa kuwa inachunguza madai kwamba watoto waliokuwa wakilelewa katika kituo kimoja kinachosimamiwa na wizara hiyo katika mkoa wa Nainawa kaskazini mwa Iraq wameuzwa kwa kundi la kigaidi la Daesh.
-
Kinara wa kundi la ISIS aangamizwa katika mkoa wa Diyala, Iraq
Jan 05, 2018 11:13Mkuu wa kamati ya usalama ya mkoa wa Diyala, nchini Iraq Bw. Sadiq al-Husseini amesema, jeshi la nchi hiyo limemuua kiongozi muhimu wa kundi la ISIS mkoani Diyala, mashariki mwa nchi hiyo.
-
Helikopta za Marekani zawaokoa viongozi wa Daesh Deir ez-Zor, Syria
Dec 30, 2017 00:57Katika kuendeleza uungaji misaada ya Marekani kwa makundi ya kigaidi na ukufurishaji la Daesh, helikopta za kivita za nchi hiyo zimeonekana usiku wa kuamkia leo zikiruka kuelekea mji wa Deir ez-Zor nchini Syria na kuwabeba viongozi kadhaa za kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) na kuwapeleka mji wa Al-Hasakah, kaskazini mashariki mwa Syria.
-
Marekani yatuma maelfu ya magaidi wa Daesh barani Ulaya
Dec 27, 2017 12:21Gazeti moja linalochapishwa nchini Marekani limeandika kuwa, Marekani na wapinzani nchini Syria wamewatuma katika nchi za Ulaya maelfu ya magaidi wa kundi la ukufurishaji la Daesh kutokea Syria.
-
Russia yatoa indhari: Kuna magaidi zaidi ya 10,000 wa DAESH (ISIS) nchini Afghanistan
Dec 24, 2017 13:10Mjumbe maalumu wa rais wa Russia nchini Afghanistan ametoa indhari kuwa wanachama zaidi ya elfu kumi wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh hivi sasa wako nchini Afghanistan na kwamba idadi yao inazidi kuongezeka kutokana na kubadilisha maskani yake kundi hilo baada ya kusambaratishwa katika nchi za Syria na Iraq.
-
Waziri wa Sheria wa Algeria: Waalgeria 226 wamejiunga na Daesh
Dec 19, 2017 04:33Waziri wa Sheria wa Algeria ametangaza kuwa raia wa nchi hiyo wasiopungua 226 wameelekea katika nchi za Iraq na Syria kwa ajili ya kujiunga na kundi la kigaidi la Daesh.
-
Marekani yaunda kundi jipya la waasi Syria
Dec 16, 2017 12:11Kituo cha Mapatano cha Russia nchini Syria kimetangaza kuwa, Marekani imeanzisha kundi jipya la waasi lililopewa jina la Jeshi Jipya la Syria katika kambi ya wakimbizi iliyoko mkoani Hasaka huko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Viongozi wa nchi za Afrika wana wasiwasi wa kurejea barani humo Madaesh wanaotoka Syria na Iraq
Dec 14, 2017 12:13Viongozi wa nchi za Afrika wamesema wana wasiwasi wa kurejea barani humo maelfu ya wanachama wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la DAESH (ISIS) kutoka nchi za Iraq na Syria.
-
Kutangazwa ushindi wa mwisho wa taifa la Iraq dhidi ya ISIS
Dec 11, 2017 00:04Mkanda wa kuendelea kushindwa kundi la kigaidi la Daesh katika eneo la Mashariki ya Kati unaendelea kiasi kwamba, muda mchache baada ya kutangazwa kushindwa kikamilifu ISIS nchini Syria, habari nyingine zinasema kuwa magaidi hao wakufurishaji wameshindwa kikamilifu pia nchini Iraq.
-
Iraq yatangaza rasmi kuangamizwa kundi la kigaidi la ISIS nchini humo
Dec 09, 2017 11:40Waziri Mkuu wa Iraq leo ametangaza rasmi kumalizika kwa mafanikio vita dhidi ya kundi la kigaidi la ISIS au Daesh nchini humo.