-
Idadi kubwa ya walioambukizwa Ebola DRC na Uganda ni wanawake na wasichana
Jun 14, 2026 03:09Wanawake na wasichana wanawakilisha asilimia 53.4 ya wagonjwa wa Ebola waliothibitishwa kwa vipimo vya maabara katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Uganda, sawa na wagonjwa 244 kati ya 457 kwa mujibu wa taarifa za wagonjwa katika maeneo zilikopatikana. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Wanawake.
-
WHO: Ebola inaenea katika maeneo mapya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Jun 13, 2026 02:37Shirika la Afya Duniani (WHO) jana Ijumaa lilitangaza kuwa mlipuko wa Ebola kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo sasa unaenea katika maeneo mapya.
-
DRC: Visa vilivyothibitishwa vya Ebola vinakaribia 600
Jun 11, 2026 11:32Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetangaza kwamba idadi ya visa vilivyothibitishwa vya Ebola imepanda na kukaribia 600, huku kukiendelezwa uhamasishaji miongoni mwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuchukua hatua za kujikinga.
-
Maandamano dhidi ya kituo cha kupambana na Ebola cha Marekani huko Kenya yageuka kuwa vurugu
Jun 09, 2026 13:42Polisi wa Kenya wametumia gesi ya kutoa machozi dhidi ya raia waliokuwa wakiandamana huko Nanyuki leo Jumanne kupinga kuanzishwa kituo cha karantini cha Marekani ndani ya kambi ya kijeshi ili kuwapokea raia wa Marekani wanaoshukiwa kuwa na Ebola.
-
Kliniki katika kitovu cha Ebola nchini DR Congo 'yazidiwa' na wagonjwa
Jun 06, 2026 11:10Ripoti zinasema kuwa, hospitali katika eneo lililoathiriwa na Ebola la Bunia katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imejaa idadi kubwa ya wagonjwa wa Ebola.
-
Wanaharakati wa haki za binadamu waandamana Nairobi kupinga kituo cha Ebola cha Marekani nchini Kenya
Jun 02, 2026 15:14Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wamefanya maandamano leo mjini Nairobi wakipinga makubaliano yaliyofikiwa kati ya serikali ya nchi hiyo na Marekani ya kuanzisha nchini Kenya kituo cha kuhifadhi Wamarekani wanaoshukiwa kuambukizwa virusi vya Ebola.
-
MSF yaonya: Mlipuko wa Ebola DR Congo ni wa kutisha sana
May 31, 2026 12:45Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limeonya kwamba mlipuko wa Ebola katika Mkoa wa Ituri nchini Kongo DR unaenea kwa kasi kubwa zaidi kuliko juhudi za kukabiliana na ugonjwa huo, huku Shirika la Afya Duniani (WHO) ikifuatilia ongezeko la dharura ya afya ya umma sambamba na kuwepo mamia ya visa vinavyoshukiwa kuwa vya Ebola.
-
Wizara ya Afya ya Kongo: Idadi ya watu wanaoshukiwa kuambukizwa Ebola imepindukia 1,000
May 29, 2026 03:01Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza kuwa idadi ya watu wanaoshukiwa kuwa na Ebola nchini humo imepindukia 1,000 huku kukiwa na ongezeko la maambukizi katika majimbo ya mashariki mwa nchi hiyo.
-
Mkutano wa India na Afrika waahirishwa kutokana na mlipuko wa Ebola
May 24, 2026 03:23Umoja wa Afrika (AU) umekubaliana na India kuahirisha mkutano uliopangwa kufanyika New Delhi kutokana na hofu ya kuenea mlipuko wa Ebola ulioua zaidi ya watu 160 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na mtu mmoja nchini Uganda jirani.
-
Mkuu wa afya barani Afrika: Mlipuko wa Ebola unatishia nchi 10 zaidi
May 24, 2026 03:21Kituo cha Afya cha Umoja wa Afrika kimetahadharisha kuwa nchi kumi za Kiafrika ziko hatarini kuathiriwa na virusi vya Ebola, mbali na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda.