-
Chanjo ya Ebola yaanza kutolewa vijijini Kongo DR
May 27, 2018 23:21Wizara ya Afya katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo leo Jumatatu inaaza kupeana chanjo ya ugonjwa hatari wa Ebola katika vijiji viwili vilivyoathiriwa na mlipuko wa sasa wa maradhi hayo.
-
Wagonjwa watatu wa Ebola watoroka karantini nchini Kongo + Sauti
May 23, 2018 10:05Wagonjwa watatu walioambukizwa ugonjwa hatari wa Ebola wametoroka eneo la karantini walimokuwa katika hospitali moja huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika mji wa Mbandaka huku madakatari wakiwa mbioni kuzuia ugonjwa huo hatari kuenea.
-
WHO: Maandalizi ya kukabiliana na mlipuko wa Ebola yameboreka zaidi sasa kuliko mwaka 2014
May 21, 2018 09:26Dakta Tedros Adhanom Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) amesema leo kuwa kuenea kwa maradhi ya Ebola katika mji mkuu huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni jambo lenye kutia hofu hata hivyo akasema kuwa maandalizi ya kukabiliana na hali ya sasa yameboreka zaidi kuliko ilivyokuwa mwaka 2014 huko Magharibi mwa Afrika wakati ulivyoripotiwa mlipuko mkubwa wa homa hiyo hatari.
-
Chanjo ya Ebola kuanza kutolewa Kongo DR kesho Jumatatu
May 20, 2018 09:59Wafanyakazi wa sekta ya afya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wataanza kupewa chanjo ya Ebola kesho Jumatatu katika juhudi za kuzuia kuenea ugonjwa huo hatari.
-
WHO yapewa idhini ya kutumia chanjo ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
May 14, 2018 22:43Maafisa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamelipatia idhini Shirika la Afya Duniani (WHO) kuingiza na kutumia nchini humo chanjo ya majaribio ya ugonjwa wa Ebola. Hayo yameelezwa jana na Dakta Tedros Adhanom Ghebreyesus Mkurugenzi Mkuu wa WHO.
-
Kongo DR na UN zatuma wataalamu kukabiliana na mlipuko wa Ebola
May 13, 2018 11:15Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na taasisi za Umoja wa Mataifa zimeanza kutuma nchini humo timu za wataalamu ili kujaribu kuzuia kuenea maambukizi ya homa ya Ebola ambayo hadi sasa inashukiwa tayari imeshawaambukiza watu zaidi ya 30.
-
WHO yatahadharisha juu ya kuibuka tena ugonjwa wa Ebola huko DRC
May 11, 2018 23:47Shirika la Afya Duniani (WHO) limetahadharisha juu ya uwezekano wa kuibuka tena ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Uganda yakumbwa tena na homa ya Marburg
Oct 20, 2017 13:18Uganda imethibitisha kufariki dunia mtu mmoja kwa homa inayoenezwa na kirusi cha Marburg, homa ambayo huambatana na kuvuja damu sawa kabisa na homa ya Ebola. Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya wa nchi hiyo.
-
Walioambukizwa Ebola waongezeka DRC, wafika 20
May 16, 2017 09:52Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC idadi ya visa vinavyoshukiwa kuwa ni Ebola imeongezeka na kufikia 20.
-
Ugonjwa wa Ebola waripotiwa DRC, watu watatu wafariki dunia
May 13, 2017 02:41Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, ugonjwa wa Ebola umezuka katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kwamba, hadi sasa watu watatu wamefariki dunia kwa ugonjwa huo hatari.