-
Serikali yadhibiti mlipuko mpya wa Ebola Kongo DR
Sep 09, 2018 02:46Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza habari ya kufanikiwa kudhibiti mlipuko mpya wa ugonjwa wa Ebola nchini humo, wiki tano baada ya kuripotiwa mlipuko wa virusi hivyo hatari.
-
WHO yasema hatua za kudhibti Ebola DRC zinafanya kazi
Sep 01, 2018 09:37Shirika la Afya Duniani WHO limesema huku hatua za kudhibiti ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zikitekelezwa, kuna hatari ya kuendelea kuenea ugonjwa huo.
-
WFP yatoa msaada wa dharura wa chakula kwa waathirika wa Ebola DRC
Aug 31, 2018 02:04Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP limeanza kutekeleza mpango wa dharura wa kugawa chakula kwa waathirika wa ugonjwa wa Ebola huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.
-
Maafa ya Ebola yaongezeka DRC
Aug 26, 2018 10:18Idadi ya watu waliopoteza maisha yao kutokana na mfumuko mpya wa homa hatari ya Ebola huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imefikia watu 67 katika mwezi huu wa Agosti pekee.
-
WHO: Mlipuko wa Ebola DRC umeshadhibitiwa lakini hatari bado ipo
Aug 24, 2018 21:51Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mlipuko mpya wa ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umeshadhibitiwa, lakini kuna uwezekano wa kutokea kesi mpya, kutokana na mazingira magumu yanayosababishwa na hali mbaya ya usalama na baadhi ya maeneo kutofikika.
-
Tanzania yakabiliwa na hatari kubwa ya mlipuko wa homa ya Ebola
Aug 22, 2018 03:09Waziri wa afya wa Tanzania Bibi Ummy Mwalimu amesema, Tanzania inakabiliwa na hatari kubwa ya kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, ambao umesababisha vifo vya watu 50 kati ya wagonjwa 91 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC
-
Idadi ya wahanga wa homa ya Ebola yaongezeka DRC
Aug 21, 2018 03:10Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilitangaza jana kwamba idadi ya wahanga wa wimbi jipya la kuenea ugonjwa wa Ebola nchini humo imeongezeka na kufikia watu 50.
-
Athari za Ebola kwa watoto DRC ni zaidi ya kuugua –UNICEF
Aug 18, 2018 02:56Watoto wanawakilisha idadi kubwa isiyo ya kawaida ya waathirika wa mlipuko wa Ebola huko mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC, limesema shirika la kuwahudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF.
-
Kongo yaanza matibabu ya majaribio kwa homa ya Ebola
Aug 15, 2018 09:30Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeanza kutumia dawa ya majaribio aina ya mAb114 kutibu mlipuko wa karibuni wa homa hiyo inayosababishwa na virusi.
-
WHO: Nchi jirani ya DRC zichukue hatua kuzuia kuenea Ebola
Aug 05, 2018 20:51Shirika la Afya Duniani WHO limesema, hali mpya ya maambukizi ya ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC inazilazimisha nchi za jirani kuchukua hatua za tahadhari ili kuzuia ungojwa huo hatari kuenea.