-
Ethiopia kumwapisha Waziri Mkuu mpya Aprili Pili
Mar 30, 2018 03:42Waziri Mkuu mteule wa Ethiopia, Abiye Ahmed ataapishwa Jumatatu ijayo. Hayo yameelezwa na Bunge la Ethiopia baada ya muungano wa chama tawala kumchagua kwa ajili ya kuziba nafasi iliyoachwa na Hailemariam Desalegn, Waziri Mkuu wa Ethiopia aliyejiuzulu.
-
UNHCR: Waethiopia waliokimbilia hifadhi Kenya wakumbwa na masaibu
Mar 29, 2018 02:01Maelfu ya wakimbizi wa Ethiopia waliokimbilia hifadhi nchi jirani ya Kenya hivi sasa wanakabiliwa na tatizo kubwa la kukidhi mahitaji yao ya msingi, limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR.
-
Ethiopia yaituhumu Eritrea kuwa inataka kuvuruga usalama wake
Mar 18, 2018 23:46Ethiopia imemtuhumu jirani yake Eritrea kuwa inataka kuvuruga usalama wake kwa kuyaunga mkono yale iliyoyaita makundi "haribifu" katika kipindi hiki ambapo sheria ya hali ya hatari inatekelezwa nchini humo.
-
Abbas Gullet: Wakimbizi wapatao 10,000 kutoka Ethiopia wameingia nchini Kenya mwezi huu pekee
Mar 17, 2018 04:22Katibu Mkuu wa Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya ametangaza kuwa, wakimbizi wapatao 10,000 kutoka Ethiopia wameingia nchini humo tangu kuanza mwezi huu wa Machi.
-
Wanafunzi 38 wapoteza maisha katika ajali ya basi Ethiopia
Mar 13, 2018 12:15Watu 38 wamepoteza maisha nchini Ethiopia baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutumbukia katika mtaro mkubwa katika jimbo la Amhara kaskazini mwa nchi hiyo.
-
Bunge la Somalia lapinga makubaliano ya Imarati na Somaliland
Mar 13, 2018 04:05Bunge la Federali la Somalia limepiga kura kwa kishindo kupinga makubaliano ya pande tatu kati ya eneo la Somaliland, Umoja wa Falme za Kiarabu na Ethiopia kuhusu bandari ya Berbera, iliyoko katika Ghuba ya Aden.
-
Jeshi la Ethiopia laua raia 9, ladai lilidhani ni waasi
Mar 12, 2018 23:14Jeshi la Ethiopia limetangaza kuua raia tisa na kuwajeruhi wengine 12 na kudai kuwa lilidhani ni waasi walio katika eneo linalopakana na Kenya.
-
Safari ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia nchini Ethiopia
Mar 09, 2018 22:00Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia amewasili Addis Ababa kwa shabaha ya kukutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Ethiopia.
-
Wananchi wa Ethiopia wafanya mgomo kulalamikia 'hali ya hatari'
Mar 06, 2018 04:33Shughuli za kawaida zimelemazwa kutokana na mgomo wa wananchi wa Ethiopia katika mji mkuu Addis Ababa na miji mingine, wanaolalamikia sheria ya hali ya hatari kwa muda wa miezi sita kufuatia kujiuzulu Waziri Mkuu Hailemariam Desalign.
-
Ethiopia yanunua hisa za Bandari ya Berbera Somaliland
Mar 02, 2018 04:21Serikali ya Ethiopia imenunua asilimia 19 ya hisa za Bandari ya Berbera iliyoko katika Jamhuri iliyojitangazia uhuru ya Somaliland nchini Somalia.