-
Misri, Sudan na Ethiopia zashindwa kuafikiana kuhusu bwawa la al-Nahdha
Apr 06, 2018 09:50Mkutano wa Misri, Sudan na Ethiopia wa kujadili suala tata la bwawa la al-Nahdha umegonga mwamba huku pande tatu hizo zikishindwa kuafikiana.
-
Hatimae Abiy Ahmed Ali awa rasmi waziri mkuu wa Ethiopia
Apr 02, 2018 21:54Abiy Ahmed Ali aliyekuwa anakaimu nafasi ya waziri mkuu wa Ethiopia baada ya maandamano ya wananchi kumlazimisha kujiuzulu waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo, Hailemariam Desalegn, jana Jumatatu aliapishwa kuwa waziri mkuu rasmi wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Zaidi ya watu 1000 watiwa mbaroni nchini Ethiopia
Mar 31, 2018 23:42Watu elfu moja na 107 wametiwa mbaroni nchini Ethiopia kwa tuhuma za kuvunja sheria za hali ya hatari nchini humo.
-
Ethiopia kumwapisha Waziri Mkuu mpya Aprili Pili
Mar 30, 2018 03:42Waziri Mkuu mteule wa Ethiopia, Abiye Ahmed ataapishwa Jumatatu ijayo. Hayo yameelezwa na Bunge la Ethiopia baada ya muungano wa chama tawala kumchagua kwa ajili ya kuziba nafasi iliyoachwa na Hailemariam Desalegn, Waziri Mkuu wa Ethiopia aliyejiuzulu.
-
UNHCR: Waethiopia waliokimbilia hifadhi Kenya wakumbwa na masaibu
Mar 29, 2018 02:01Maelfu ya wakimbizi wa Ethiopia waliokimbilia hifadhi nchi jirani ya Kenya hivi sasa wanakabiliwa na tatizo kubwa la kukidhi mahitaji yao ya msingi, limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR.
-
Ethiopia yaituhumu Eritrea kuwa inataka kuvuruga usalama wake
Mar 18, 2018 23:46Ethiopia imemtuhumu jirani yake Eritrea kuwa inataka kuvuruga usalama wake kwa kuyaunga mkono yale iliyoyaita makundi "haribifu" katika kipindi hiki ambapo sheria ya hali ya hatari inatekelezwa nchini humo.
-
Abbas Gullet: Wakimbizi wapatao 10,000 kutoka Ethiopia wameingia nchini Kenya mwezi huu pekee
Mar 17, 2018 04:22Katibu Mkuu wa Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Kenya ametangaza kuwa, wakimbizi wapatao 10,000 kutoka Ethiopia wameingia nchini humo tangu kuanza mwezi huu wa Machi.
-
Wanafunzi 38 wapoteza maisha katika ajali ya basi Ethiopia
Mar 13, 2018 12:15Watu 38 wamepoteza maisha nchini Ethiopia baada ya basi walilokuwa wakisafiria kutumbukia katika mtaro mkubwa katika jimbo la Amhara kaskazini mwa nchi hiyo.
-
Bunge la Somalia lapinga makubaliano ya Imarati na Somaliland
Mar 13, 2018 04:05Bunge la Federali la Somalia limepiga kura kwa kishindo kupinga makubaliano ya pande tatu kati ya eneo la Somaliland, Umoja wa Falme za Kiarabu na Ethiopia kuhusu bandari ya Berbera, iliyoko katika Ghuba ya Aden.
-
Jeshi la Ethiopia laua raia 9, ladai lilidhani ni waasi
Mar 12, 2018 23:14Jeshi la Ethiopia limetangaza kuua raia tisa na kuwajeruhi wengine 12 na kudai kuwa lilidhani ni waasi walio katika eneo linalopakana na Kenya.