-
Baraza la Usalama UN lalaani mashambulizi ya Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran, Damascus
Apr 03, 2024 07:19Wawakilishi waliohudhuria kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran huko Damascus (mji mkuu wa Syria) wamelaani kitendo hicho cha kinyama cha Wazayuni.
-
Baraza la Usalama laitisha kikao cha dharura kuhusu shambulio la Israel kwenye ubalozi wa Iran
Apr 03, 2024 03:39Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeitisha kikao cha dharura cha kujadili shambulizi la kigaidi la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria kikao ambacho kimeshuhudia kulaaniwa vikali Israel kwa shambulio lake hilo la kigaidii.
-
Katibu Mkuu wa UN alaani shambulio la Israel lililolenga ubalozi mdogo wa Iran Damascus
Apr 02, 2024 23:15Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani shambulio la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya sehemu ya ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria na kuonya kwamba mahesabu yoyote ya kimakosa yanaweza kusababisha mapigano yenye wigo mpana zaidi katika eneo hili tete na lisilo na uthabiti na kusababisha matokeo haribifu kwa raia.
-
Utawala wa Kizayuni washambulia jengo la ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria
Apr 01, 2024 23:23Utawala ghasibu wa Kizayuni umetekeleza shambulio la anga dhidi ya jengo la ubalozi mdogo wa Iran karibu na ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran huko Damascus Syria.
-
Iran: Uchunguzi wa kimataifa ufanyike kuhusu jinai ilizofanya Israel katika Hospitali ya Al-Shifa
Apr 01, 2024 23:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitizia ulazima wa kufanyika uchunguzi wa kimataifa kuhusiana na uharibifu, utesaji na mauaji yaliyofanywa na jeshi la Kizayuni katika Hospitali ya Al-Shifa huko Ukanda wa Ghaza.
-
Ayatullah Khatami: Siku ya Quds itakuwa tofauti kabisa mwaka huu
Mar 29, 2024 08:42Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa hapa Tehran hii leo ameashiria jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na kusema kuwa, hadithi ya Siku ya Kimataifa ya Quds mwaka huu, itakuwa hadithi tofauti kabisa kutokana na hamasa na wingi wa watu watakaoshiriki matembezi ya siku hiyo.
-
Iran: Walimwengu wana wajibu wa kuubebesha dhima utawala wa Kizayuni
Mar 28, 2024 23:09Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameitaka jamii ya kimataifa ichukue hatua na kuubebesha dhima utawala wa Kizayuni, baada ya Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Masuala ya Palestina kufanya tathmini ambayo imezitaja jinai za utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Gaza kuwa ni mauaji ya kimbari.
-
Iran yazitaka IPU, NAM kufanya juhudi za kusitisha vita Gaza
Mar 27, 2024 04:11Iran imetoa mwito kwa Jumuiya ya Kimataifa ya Mabunge (IPU) na Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (NAM) kuchukua hatua za maana na za kivitendo kusitisha mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akosoa undumakuwili wa Magharibi
Mar 26, 2024 04:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumza kwa simu na mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Ulaya katika Masuala ya Nje na Sera ya Usalama na kukosoa vikali vigezo vya undumakuwili na vinavyokinzana vya nchi za Magharibi mkabala wa Palestina na Gaza.
-
Mkutano wa Umoja wa Mabunge unaendelea Geneva kwa kuhudhuriwa na Iran
Mar 25, 2024 08:31Mkutano wa Umoja wa Mabunge Duniani, kama chombo kikubwa zaidi cha utungaji sheria chenye nchi wanachama zaidi ya 180, ukiwemo ujumbe kutoka Iran unafanyika mjini Geneva Uswisi kwa kauli mbiu ya "Diplomasia ya Bunge, Ujenzi wa Daraja la Amani na Maelewano".