-
Iran yakaribisha hatua ya Waarabu ya kuhuisha uhusiano na Syria
Feb 28, 2023 23:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amepongeza hatua ya nchi za Kiarabu ya kuhuisha na kuimarisha uhusiano na Damascus, akisisitiza kuwa mkondo huo mpya wa kurejea mataifa ya Kiarabu nchini Syria unaonyesha kuporomoka kwa njama za nchi za Magharibi.
-
Iran kuanza kuuza bidhaa za nyuklia nje ya nchi
Feb 26, 2023 08:11Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) ametangaza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu inajiandaa kuanza kusafirisha nje ya nchi bidhaa zake za nyuklia, zikiwemo za tiba.
-
Mahusiano ya pande mbili ya Iran na Iraq; mhimili wa mazungumzo ya Amir-Abdollahian mjini Baghdad
Feb 24, 2023 09:49Waziri wa Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye yuko safarini nchini Iraq amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali wa nchi hiyo akiwemo Rais na Waziri Mkuu na kujadili uhusiano wa pande mbili na wa kieneo.
-
Iran: Kusambaratika Israel hakuepukiki licha ya uungaji mkono wa US
Feb 23, 2023 23:37Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema utawala haramu wa Israel upo katika ncha ya kusambaratika na kutokomea, licha ya uungaji mkono.
-
Kuwasili nchini Iran ujumbe wa kiuchumi wa Senegal
Feb 23, 2023 04:07Ujumbe wa ngazi ya juu wa kiuchumi wa Senegal ukiongozwa na mshauri mkuu wa rais na mkuu wa chama cha wafanyakazi cha nchi hiyo umeasili mjini Tehran.
-
Haki za binadamu ni mhanga wa siasa za nchi za Magharibi
Feb 23, 2023 03:39Mkuu wa Masuala ya Kimataifa ambaye pia ni Katibu wa Idara ya Masuala ya Haki za Binadamu ya Iran, amesema siasa zinadhuru pakubwa suala zima la haki za binadamu na kuongeza kuwa vyombo vya habari vinapaswa kuheshimu misingi ya tasnia ya uandishi habari na kubainisha ukweli wa mambo mbali kabisa na mifungamano ya kisiasa.
-
Mkuu wa Kikosi cha Quds cha IRGC: Iran imezuia njama za Marekani za kudhibiti Asia Magharibi
Feb 22, 2023 23:03Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa, Iran imefanikiwa kukwamisha majaribio ya Marekani ya kutaka kujikita katika eneo la Magharibi mwa Asia na kuyaweka mataifa ya eneo hilo chini ya udhibiti wake.
-
Iran inajiandaa kujibu mapigo ya kuwekewa vikwazo na Umoja wa Ulaya
Feb 21, 2023 00:09Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema ndani ya siku chache zijazo itatoa jibu la vikwazo vya hivi karibuni vilivyowekwa na Umoja wa Ulaya dhidi ya shakhsia 32 na taasisi mbili za Jamhuri ya Kiislamu.
-
Jibu kali la Iran kwa taarifa ya pamoja ya US na Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi
Feb 18, 2023 22:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametupilia mbali maelezo yaliyomo kwenye taarifa ya kikao cha tatu cha jopo kazi la pamoja la Marekani na Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (GCC) kuhusu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, na kueleza kwamba kutolewa taarifa kama hiyo kunaendana na mkakati wa muda mrefu wa utawala wa Marekani wa kuzusha mfarakano kati ya nchi za eneo hili.
-
Kiongozi Muadhamu azikosoa nchi za Waislamu kwa kufumbia macho kadhia ya Palestina
Feb 18, 2023 07:28Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amezikosoa nchi za Kiislamu kwa kutochokua hatua yoyote ya maana juu ya kadhia ya Palestina.