-
Raisi: Vikwazo vipya vinaonesha Iran ina haki ya kutoiamini Marekani
Jun 17, 2022 07:25Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema hatua ya Marekani kwa upande mmoja kudai kuwa ina nia ya kweli ya kufanya mazungumzo na Iran na wakati huohuo inatangaza vikwazo vipya dhidi ya taifa hili kwa upande mwingine, inaonesha wazi kuwa Tehran ina haki kutoiamini Washington.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu juu ya kuimarishwa mahusiano ya Iran na Turkmenistan
Jun 16, 2022 04:58Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kislamu alisema Jumatano ya jana wakati alipokutana na Rais Serdar Berdimuhamedow wa Turkmenistan na ujumbe aliofutana nao kwamba, kustawisha na kuimarishwa kadiri inavyowezekana uhusiano wa Iran na Turkmenistan ni kwa maslahi ya nchi mbili.
-
Iran yamuonya mkuu wa IAEA asifanye 'mambo kuwa magumu'
Jun 15, 2022 22:51Msemaji wa Shirika la Atomiki la Iran amemshauri Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) kujizuia kufanya mambo kuwa magumu kwa kutoa matamshi ya kisiasa.
-
Kiongozi Muadhamu: Sera za Iran zinatoa kipaumbele juu ya kuimarisha uhusiano na majirani
Jun 15, 2022 07:57Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kipaumbele katika sera za kigeni za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hivi sasa ni kuimarisha uhusiano na mataifa jirani.
-
Raisi: Iran na Turkmenistan zina uhusiano uliokita mizizi
Jun 15, 2022 07:55Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uhusiano wa pande mbili wa nchi hii na Turkmenistan ni wa kidugu na uliokita mizizi.
-
Kauli zisizo za kirafiki za Fuad Hussein; ulazima wa kutoa ufafanuzi uko kwa Iran au Iraq?
Jun 15, 2022 03:39Waziri wa mambo ya nje wa Iraq, kwa mara ya kwanza ametoa matamshi ya kuituhumu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwamba inaingilia masuala ya ndani ya nchi yake na kudai kuwa uhusiano wa Iran na Iraq umetoka kwenye hatua ya "ukimya" na kufikia hatua ya kuhitajika "ufafanuzi".
-
Wabunge wa Iran: IAEA imepoteza itibari ya kiufundi
Jun 13, 2022 06:28Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) imesema hatua ya Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) ya kupasisha azimio dhidi ya Iran imeonesha wazi kuwa taasisi hiyo ya Umoja wa Mataifa imepoteza itibari yake ya kiufundi.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu kuwa mapambano ndio njia pekee ya kufikia ushindi dhidi ya Marekani
Jun 12, 2022 04:33Akizungumza jana Jumamosi alasiri katika kikao na Rais Nicolas Maduro wa Venezuela na ujumbe alioandamana nao, Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya kusimama imara Iran na Venezuela mbele ya mashinikizo makali na vita vya pande kadhaa vya Marekani na kusisitiza: Uzoefu wa mafanikio wa nchi mbili unaonyesha kwamba njia pekee ya kukabiliana na mashinikizo hayo ni mapambano na kusimamam imara.
-
Kundi la kwanza la mahujaji wa Kiirani laondoka nchini kwenda Saudia
Jun 12, 2022 03:27Kundi la kwanza la wananchi wa Iran wanaokwenda kutekeleza ibada tukufu ya Hija limeondoka nchini mapema leo Jumapili kwenda katika mji mtukufu wa Madina nchini Saudi Arabia.
-
Abdollahian: Azimio la IAEA dhidi ya Iran lilichochewa kisiasa
Jun 12, 2022 03:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezikosoa vikali Marekani na nchi tatu za Ulaya za Uingereza, Ufaransa na Ujerumani, kwa kuwasilisha azimio dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu mbele ya Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA.