-
Papa Francis: Iran ni nchi yenye utamaduni tajiri na ustaarabu mkubwa
Nov 01, 2018 12:52Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amesema, sifa kubwa maalumu ya taifa la Iran ni kuwa kwake na utamaduni tajiri wa kiutu ambao unaweza kutumiwa kwa ajili ya kumuokoa mwanadamu wa zama hizi.
-
NYT: Trump atafeli katika sera zake za vikwazo dhidi ya Iran
Nov 01, 2018 03:26Gazeti la New York Times la Marekani limeandika kuwa sera za Rais Trump wa Marekani za kuiwekea vikwazo Iran zitafeli.
-
Zarif: Mossad inatekeleza njama za kuvuruga uhusiano wa Iran na EU
Nov 01, 2018 03:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema madai ya Denmark dhidi ya Iran ni katika fremu ya oparesheni ya upotoshaji inayotekelezwa na shirika la kijasusi la utawala wa Kizayuni wa Israel linalojulikana kama Mossad.
-
Rais Rouhani: Marekani itafeli tu katika njama zake mpya dhidi ya Iran
Oct 31, 2018 12:22Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, licha ya kuwepo vikwazo vya Marekani dhidi ya Tehran, lakini nchi nyingi duniani za Asia na Ulaya zina hamu ya kuendeleza ushirikiano wao na Iran.
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran aelekea Najaf Iraq kushiriki maandamano ya Arubaini
Oct 30, 2018 01:15Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo anaelekea mjini Najaf, Iraq, kwa ajili ya kushiriki katika maandamano ya Arubaini ya Imam Husain AS na pia kufanya ziara katika Haram tukufu ya Imam Ali AS.
-
Arubaini ya Imam Hussein AS inabeba ujumbe wa umoja na mshikamano wa Waislamu
Oct 28, 2018 04:38Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) amesema Arubaini ya Imam Hussein AS inabeba ujumbe muhimu wa mahaba, umoja na mshikamano wa Waislamu kote duniani mbele ya madola ya kibeberu.
-
Uganda yaomba kushirikiana zaidi na Iran katika sekta ya kilimo
Oct 27, 2018 12:11Waziri wa Kilimo wa Uganda Vincent Ssempijja amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina uwezo mkubwa katika sekta ya kilimo, hivyo ametaka mashirika ya kilimo ya Iran yawekeze nchini humo na pande mbili kushirikiana zaidi katika miradi ya kilimo.
-
Trump azidi kupata pigo; Iran na Ulaya kufungua kanali maalumu ya mabadilishano ya fedha za kigeni
Oct 27, 2018 04:03Siasa za Marekani za kuiwekea vikwazo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimezidi kupata pigo baada ya nchi za Ulaya na Tehran kuamua kufungua kanali maalumu ya kifedha kwa ajili ya wasafirishaji nje bidhaa wa pande hizi mbili.
-
Iran: Trump ni mwanagenzi wa hali ya Mashariki ya Kati
Oct 26, 2018 21:52Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, rais wa Marekani, Donald Trump ni mwanagenzi na hana welewa wa kutosha kuhusu hali ya Mashariki ya Kati wala historia, sifa maalumu za watu wake na pia matukio ya miaka ya hivi karibuni ya eneo hili.
-
"Uwezo wa kujihami Iran ni kwa maslahi ya kuzuia vita Mashariki ya Kati"
Oct 26, 2018 11:49Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amesema stratijia ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kuimarisha uwezo wake wa kujihami ni kwa shabaha ya kuzuia vita katika eneo hili la Mashariki ya Kati.