-
Jeshi la Anga la Iran laanza mazoezi makubwa kati mwa nchi
Nov 01, 2017 01:01Jeshi la Anga la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limeanzisha mazoezi makubwa yanayojumuisha ndege aina mbali mbali za kivita katika eneo la Isfahan, kati mwa Iran.
-
Rais Rouhani: Wamarekani wanataka kuwavunja moyo wananchi wa Iran
Oct 31, 2017 01:14Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Wamarekani wanataka kuwavunja moyo wananchi wa Iran kuhusu masuala yao ya kiuchumi na hiyo ndiyo njama yao kuu ya kuzuia maendeleo ya taifa hili.
-
Amir wa Qatar: Iran ndio njia pekee ya kupitishia chakula na dawa katika kipindi cha mzingiro
Oct 30, 2017 23:16Mfalme wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani amesema Iran ndio njia pekee ya kupitishia chakula kwa ajili ya wananchi wa Qatar waliowekewa mzingiro; na akaongeza kwamba Saudi Arabia na nchi nyengine tatu za Kiarabu zinakula njama ya kuubadilisha utawala katika nchi yake.
-
Iran itaendelea kushirikiana na IAEA, kufungamana na JCPOA
Oct 30, 2017 04:30Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema kuna haja Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) uendelee kuwa chombo huru na kisichoegemea upande wowote akisisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kuimarisha ushirikiano wake na wakala huo.
-
Iran itashiriki vilivyo katika kuijenga upya Syria
Oct 30, 2017 00:30Waziri wa Viwanda, Madini na Biashara wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran itashiriki vilivyo katika utekelezaji wa mipango itakayoainishwa na serikali ya Syria katika kujenga upya sekta mbali za uzalishaji, utoaji huduma na ustawi zilizoharibiwa vibaya na magenge ya kigaidi yaliyoivamia nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Rouhani: Wamarekani wametiwa kiwewe na uwezo mkubwa wa makombora wa Iran
Oct 29, 2017 12:41Rais Hassan Rouhani ameutaja kuwa ni kichekesho na dhihaka mwito wa Marekani wa kutaka kufanyika mazungumzo mapya kuhusu makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kusisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itaendelea kuzalisha makombora kwa ajili ya kujilinda.
-
Ayatullah Shirazi: Waislamu wasinyamazie kimya jinai dhidi ya wenzao wa Rohingya
Oct 29, 2017 12:32Ayatullah Makarim Shirazi ambaye ni miongoni mwa wanazuoni wakubwa wa Kiislamu nchini Iran ameeleza kusikitishwa kwake na hali mbaya inayozidi kuwakabili Waislamu wa jamii ya Rohingya huku akiwataka Waislamu kote duniani kutofumbia macho jinai wazofanyia ndugu zao nchini Myanmar.
-
IAEA: Iran imeheshimu makubaliano ya nyuklia ya JCPOA
Oct 29, 2017 12:23Kwa mara nyingine tena Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) amesema kuwa Iran imefungamana na kutekeleza wajibu na majukumu yake kuhusu makubaliano ya nyuklia maarufu kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA).
-
UN yapitisha azimio lililopendekezwa na Iran la kutokomeza silaha za nyuklia
Oct 29, 2017 00:14Azimio lililopendekezwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa kuhusiana na kutokomezwa silaha za nyuklia limepitishwa katika Kamati ya Utokomezaji Silaha ya Baraza Kuu la umoja huo kwa kura 112 za 'ndiyo' licha ya upinzani wa Marekani na waitifaki wake.
-
Kongamano la kiuchumi na uwekezaji baina ya Iran na Afrika kuanza leo Tehran
Oct 28, 2017 23:35Kongamano la kiuchumi na uwekezaji baina ya Iran na Afrika linafanyika leo mjini Tehran huku zaidi ya washiriki 600 wakitazamiwa kuhudhuria kutoka sekta binafsi za pande mbili. Aidha maafisa wa serikali za Afrika na Iran watahudhuria kongamano hilo.