-
Afrika Kusini kupunguza kiwango cha uhusiano wake na utawala wa Kizayuni wa Israel
Mar 08, 2023 03:09Bunge la Afrika Kusini jana Jumanne lilipiga kura ya kuunga mkono kushushwa hadhi ya ubalozi wa nchi hiyo huko Israel kutokana na kuendelea unyanyasaji na mauaji ya utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Mash'al: Kuanzisha uhusiano na Israel umeisababishia Palestina dhiki
Mar 05, 2023 07:28Kiongozi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) nje ya nchi ameyakosoa baadhi ya madola ya Kiarabu kwa kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel na kusisitiza kuwa, ushirikiano na utawala huo wa Kizayuni haujakuwa na matokeo mengine ghairi ya kuwasababishia Wapalestina dhiki na matatizo.
-
"Mkutano wa Aqaba unaipa Israel kibali cha kushadidisha jinai dhidi ya Wapalestina"
Feb 27, 2023 06:13Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameashiria mkutano eti wa kiusalama ulioandaliwa na Marekani huko Jordan na kusisitiza kuwa, kikao hicho cha Aqaba kinalenga kuupa utawala wa Kizayuni wa Israel ridhaa ya kushadidisha jinai zake dhidi ya Wapalestina.
-
Iran: Kusambaratika Israel hakuepukiki licha ya uungaji mkono wa US
Feb 23, 2023 23:37Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema utawala haramu wa Israel upo katika ncha ya kusambaratika na kutokomea, licha ya uungaji mkono.
-
Oman yaruhusu ndege za Israel zitumie anga yake
Feb 23, 2023 23:36Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel amedai kuwa, Oman imeidhinisha ndege za utawala huo haramu kuruka katika anga ya nchi hiyo ya Ghuba ya Uajemi.
-
Baraza la Usalama lalaani ujenzi wa vitongoji haramu Palestina inayokaliwa kwa mabavu
Feb 21, 2023 03:51Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha rasimu ya azimio linalolaani uamuzi wa serikali ya Israel yenye misimamo ya kufurutu ada ya Benjamin Netanyahu wa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya tisa katika ardhi za Wapalestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Nchi za Amerika ya Latini zalaani ujenzi wa vitongoji haramu
Feb 18, 2023 06:23Kundi la nchi za Amerika ya Latini limelaani na kukosoa vikali uamuzi wa serikali ya Israel yenye misimamo ya kufurutu ada ya Benjamin Netanyahu wa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya tisa katika ardhi za Wapalestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Rasimu ya azimio la Umoja wa Mataifa yaitaka Israel kukomesha mara moja upanuzi wa vitongoji haramu
Feb 18, 2023 00:03Rasimu ya azimio jipya la Umoja wa Mataifa ambayo inasubiri kupigiwa kura inautaka utawala ghasibu wa Israel kukomesha haraka iwezekanavyo shughuli za upanuzi wa vitongoji vya walowezi katika ardhi za Palestina unazozikalia kwa mabavu.
-
Wanachuo wa Sudan wapinga uhusiano wa kawaida na Israel
Feb 14, 2023 04:32Wanafunzi wa Vyuo Vikuu nchini Sudan wamefanya maandamano katika mji mkuu Khartoum kupinga hatua ya utawala wa kijeshi wa nchi hiyo ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Meya wa Barcelona avunja uhusiano na Israel, aitetea Palestina
Feb 09, 2023 22:55Jiji la Barcelona la kaskazini mashariki mwa Uhispania limetangaza kusimamisha uhusiano wake na utawala haramu wa Israel.