-
Hizbullah: Tumefanikiwa kuangamiza wanajeshi 95 wa Israel
Nov 01, 2024 07:00Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon imesema zaidi ya maafisa na wanajeshi 95 wa Israel wameuawa na wengine wasiopungua 900 wamejeruhiwa tangu utawala huo ghasibu uanzishe operesheni ya nchi kavu dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Ubunifu mpya wa kisheria wa Afrika Kusini katika kuwatetea Wapalestina
Oct 31, 2024 07:36Kuendelea mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza kumeifanya timu ya wanasheria wa Afrika Kusini kuwasilisha kesi inayokaribia kurasa 5,000 dhidi ya utawala katili wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ).
-
Iran: Tutajibu iwapo Israel itarusha hata mshale jangwani
Oct 30, 2024 23:07Vyombo vya ulinzi vya Iran vimesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo ya uchokozi wowote wa Israel dhidi ya ardhi yake, hata kama hatua hiyo ni ndogo na isiyo na tija, kama kurusha mshale kuelekea kwenye jangwa moja la nchi hii.
-
Sheikh Qassem: Hizbullah itazima 'mpango mkubwa' wa Israel katika eneo
Oct 30, 2024 23:07Katibu Mkuu mpya wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon amesema kundi hilo la mapambano ya Kiislamu litaendelea kupambana kwa shabaha ya kusambaratisha njama za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya eneo zima la Asia Magharibi.
-
Malalamiko ya wajumbe wa Baraza la Usalama dhidi ya ushirikiano wa Marekani na utawala wa Kizayuni
Oct 30, 2024 06:35Katika kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kilichofanyika karibuni kwa ajili ya kijadili suala la hujuma ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, nchi nyingi zikiwemo Algeria, China, Russia, Iraq na Syria zimelaani vikali kitendo hicho cha uchokozi na kutaka uchokozi huo ukomeshwe mara moja.
-
Iran: Tuna haki halali ya kujilinda na kujihami
Oct 30, 2024 00:00Msemaji wa serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani amesema Jamhuri ya Kiislamu ina haki ya kujilinda na kusisitiza kuwa, nchi hii itatekeleza haki hiyo "halali" kwa "wakati na mahali mwafaka."
-
Israel yauwa raia wasiopungua 93 katika hujuma ya umwagaji damu huko Bait Lahia
Oct 29, 2024 08:49Ndege za kivita za Israel zimeshambulia kwa mabomu jengo la makazi ya raia linalowahifadhi Wapalestina waliolazimika kuhama makazi yao kaskazini mwa Ukanda wa Gaza na kuua makumi ya watu na kujeruhi wengine wengi.
-
Kushiriki Marekani kwa 70% katika jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel
Oct 29, 2024 04:20Takwimu rasmi za makadirio zilizochapishwa zinaonyesha kuwa, Marekani imetoa zaidi ya dola bilioni 22 za silaha na misaada ya kijeshi kwa utawala wa Kizayuni wa Israel katika kipindi cha mwaka mmoja tu uliopita.
-
Rais Pezeshkian: Wairani watajibu chokochoko za maadui dhidi ya nchi yao
Oct 26, 2024 23:40Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian ametoa rambirambi zake kufuatia kuuawa shahidi maafisa usalama wa nchi hii katika mashambulizi ya kichokozi ya jana Jumamosi ya utawala wa Kizayuni na kundi la kigaidi linaloungwa mkono na maajinabi.
-
Tehran: Tuna haki halali ya kujihami mkabala wa uvamizi wa Wazayuni
Oct 26, 2024 07:22Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali hatua ya kichokozi ya utawala wa Kizayuni ya kushambulia baadhi ya vituo vya kijeshi hapa nchini, na kuitaja kuwa ni ukiukwaji wa wazi wa sheria za kimataifa na Mkataba wa Umoja wa Mataifa.