-
Kiongozi Muadhamu: Israel ilifanya makosa, 'itaadhibiwa' kwa kushambulia ubalozi mdogo wa Iran
Apr 10, 2024 04:22Kiongozi Muadhamu wa wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei anasema utawala wa Kizayuni wa Israel "lazima uadhibiwe na kutiwa adabu" kwa shambulio lake baya dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran katika mji mkuu wa Syria, Damascus.
-
Kuongezeka mashinikizo dhidi ya serikali ya Biden kwa ajili ya kupungaza uungaji mkono wake kwa utawala wa Kizayuni
Apr 07, 2024 03:37Kuendelea vita vya Ghaza na jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wasiokuwa na hatia wa eneo hilo na hasa mauaji ya kimbari na utumiaji njaa kama silaha, kumezidisha mashinikizo ya ndani kwa serikali ya Biden ya kumtaka apunguze uungaji mkono wake kwa Tel Aviv, na wakati huo huo, kuongeza pia tofauti kati ya Ikulu ya White House na Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni.
-
Kwa miongo saba, Marekani imeipatia Israel msaada wa dola bilioni 300
Apr 07, 2024 03:34Jopo la wanafikra la Baraza la Uhusiano wa Nje la Marekani limetoa ripoti kuhusu kiwango cha msaada wa karibu dola bilioni 300 ambazo Washington, ikiwa ndiye muungaji mkono mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, imetoa katika muda wa miongo saba kuupatia utawala huo.
-
OCHA: Tangu Oktoba 7, Israel imefanya mashambulio zaidi ya 700 Ukingo wa Magharibi na kuua watu 428
Apr 05, 2024 23:08Ukiwa unakaribia kutimia mwezi wa sita tangu utawala haramu wa Kizayuni wa Israel ulipoanzisha vita vya kinyama na mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza, Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, katika kipindi hicho, zaidi ya mashambulizi 700 yamefanywa na utawala huo ghasibu dhidi ya Wapalestina wa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu ikiwemo Baitul Muqaddas Mashariki.
-
Wanajeshi wa Israel wazuiliwa kwenda livu ya nyumbani kwa tahadhari na hofu ya shambulio la Iran
Apr 04, 2024 22:53Jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel limesitisha livu ya nyumbani kwa wanajeshi wake kutokana na kuwepo hofu inayoongezeka ya utawala huo kuandamwa na shambulio la kulipiza kisasi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Iran kufuatia shambulio la kigaidi ulilofanya wiki hii kwenye ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria.
-
Wanasheria zaidi ya 600 waionya Uingereza: Kuipatia silaha Israel ni ukiukaji wa sheria za kimataifa
Apr 04, 2024 22:49Zaidi ya wanasheria 600 wa Uingereza, wakiwemo majaji watatu wa zamani wa Mahakama ya Juu, mawakili, wasomi, na majaji wakuu wastaafu, wameonya kwamba hatua ya serikali ya Uingereza ya kuupatia silaha utawala wa Kizayuni wa Israel inakiuka sheria za kimataifa.
-
Baraza la Usalama laitisha kikao cha dharura kuhusu shambulio la Israel kwenye ubalozi wa Iran
Apr 03, 2024 03:39Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeitisha kikao cha dharura cha kujadili shambulizi la kigaidi la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus Syria kikao ambacho kimeshuhudia kulaaniwa vikali Israel kwa shambulio lake hilo la kigaidii.
-
Baada ya kufanya unyama mkubwa kwa majuma 2, jeshi la Israel laondoka Hospitali ya Al-Shifa
Apr 01, 2024 23:19Jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel limeondoka ndani ya Hospitali ya Al-Shifa na maeneo ya jirani magharibi mwa Mji wa Ghaza mapema jana Jumatatu na kuacha majeruhi wengi na uharibifu mkubwa katika hospitali hiyo na viunga vyake.
-
Askari wa Israel wakiri, wengi waliowaua Ghaza kama 'magaidi' ni raia wa kawaida
Apr 01, 2024 23:18Maafisa na askari wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel wamekiri kuwa akthari ya vifo vilivyoelezewa na jeshi hilo kuwa ni vya kuua "magaidi" wakati wa vita vyake dhidi ya Ukanda wa Ghaza, kiukweli hasa ni vya mauaji ya raia wa kawaida.
-
Hamas: Kuanzisha maeneo ya kunyonga watu huko Gaza ni uhalifu wa kikatili wa kivita
Apr 01, 2024 07:52Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kwamba, kilichofichuliwa na vyombo vya habari vya Israel kuhusu hatua ya jeshi la utawala huo ya kuanzishwa "maeneo ya kunyonga watu" katika Ukanda wa Gaza, ambapo mtu yeyote anayetembea katika maeneo hayo anauawa, ni jinai ya kikatili ya kivita.