Aug 17, 2022 12:13
Burundi imekuwa nchi ya kwanza kutuma wanajeshi wake katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kufuatia uamuzi wa karibuni hivi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wa kutuma kikosi cha pamoja cha kieneo katika nchi hiyo ili kwenda kupambana na magenge ya waasi na wanamgambo.