-
Wafuasi wa Fayulu walioshindwa katika uchaguzi DRC wakutana Ubelgiji na kuunda chama kipya + Sauti
Mar 24, 2019 12:15Viongozi wa Jukwaa la Lamuka ambao waliungana kumuunga mkono Martin Fayulu kama mgombea kiti cha urais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika uchaguzi uliopita na kisha mgombea huyo kushindwa, sasa wamekutana Ubelgiji na kugeuza jukwaa hilo kuwa chama cha kisiasa kikiongozwa na Fayulu. Mwandishi wetu Mosi Mwasi na maelezo zaidi...
-
Maafisa wa Tume ya Uchaguzi DRC wakanusha madai ya ufisadi ya Marekani
Mar 24, 2019 03:05Mwenyekiti wa Tume Huru ya Kitaifa ya Uchaguzi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo CENI, Corneille Nangaa pamoja na maafisa wengine wawili wa ngazi za juu wa tume hiyo wamekanusha vikali madai ya Marekani kwamba walihusika katika ufujaji wa fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya uchaguzi uliopita nchini humo.
-
UN: DRC inahitaji dola bilioni 1.6 kwa ajili ya misaada ya kibinadamu
Mar 21, 2019 20:47Umoja wa Mataifa umesema unahitaji msaada wa dola bilioni 1.65 za Marekani kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya msingi na ya kibinadamu ya watu milioni 9 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, walioathiriwa na mapigano.
-
Ajali ya treni yaua na kujeruhi zaidi ya watu 130 DRC
Mar 19, 2019 02:30Ajali ya garimoshi la kusafirishia mizigo iliyotokea siku ya Jumapili katika mkoa wa Kasai wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesababisha kupoteza maisha zaidi ya watu 50 na kujeruhiwa wengine wapatao 80.
-
Rais Felix Tshisekedi wa DRC awaachia huru mamia ya wafungwa wa kisiasa
Mar 14, 2019 10:35Rais mpya wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Félix Tshisekedi amesaini dikrii ya kuwaachia huru mamia ya wafungwa wa kisiasa.
-
UN: Mauaji ya watu zaidi ya 500 DRC ni jinai dhidi ya binadamu
Mar 12, 2019 22:56Umoja wa Mataifa umesema mauaji ya zaidi ya watu 500 huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) yanaweza kuhesabiwa kuwa jinai dhidi ya binadamu.
-
Ugonjwa angamizi wa tauni waibuka mpaka wa Uganda na DRC
Mar 12, 2019 13:01Ugonjwa angamizi wa tauni umeibuka katika mpaka wa Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambapo hadi sasa watu kadhaa wanaripotiwa kupoteza maisha.
-
Bemba ataka ICC impe fidia kwa kumfunga miaka 10 bila hatia
Mar 12, 2019 04:26Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jean-Pierre Bemba, ambaye Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC mwaka jana ilimuondoa hatiani, anaitaka mahakama hiyo ya mjini The Hague nchini Uholanzi impe fidia ya Yuro milioni 68 kwa kutompata na hatia katika kesi ya jinai za kivita iliyokuwa ikimuandama.
-
Guterres ataka kupunguzwa wanajeshi 2000 wa Monusco waliopo Kongo
Mar 10, 2019 10:32Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametaka kupunguzwa wanajeshi elfu mbili wa kikosi cha kulinda amani cha umoja huo waliopo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (Monusco).
-
Mshindi wa Tuzo ya Nobel akosoa serikali ya umoja wa kitaifa DRC
Mar 10, 2019 10:17Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel ameitaja kama usaliti kwa wananchi, hatua ya Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kukubaliana na mtangulizi wake, Joseph Kabila kuunda serikali ya umoja wa kitaifa katika nchi hiyo.