-
Uchaguzi wa Kongo DR na kuendelea mivutano ya kisiasa
Jan 12, 2019 14:41Siku ya Alkhamisi Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (CENI) ilimtangaza Felix Tshisekedi kuwa mshindi wa kiti cha urais baada ya kujinyakulia asilimia 38.57 ya kura.
-
SAUTI, Wakongomani waendelea kushangazwa na ushindi wa Felix Tshisekedi licha ya kwamba ni mpinzani
Jan 12, 2019 13:52Hali ya suitafahamu imeendelea kutawala nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kufuatia kutangazwa Felix Tshisekedi kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliopita.
-
Vyama vinavyomuunga mkono Kabila vyanyakua viti vingi vya Bunge la Kongo DR
Jan 12, 2019 04:20Vyama vya siasa vinavyomuunga mkono rais anayeondoka madarakani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila vimenyakua viti vingi katika uchaguzi wa Bunge.
-
Fayulu asema alipata 61% ya kura, kwenda mahakamani leo kupinga matokeo ya CENI
Jan 12, 2019 00:00Martin Fayulu, mgombea wa muungano wa upinzani wa Lamuka katika uchaguzi wa rais katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa yeye ndiye aliyeibuka mshindi katika uchaguzi huo kwa kupata asilimia 61 ya kura, huku akitazamiwa hii leo kwenda katika Mahakama ya Katiba kupinga matokeo yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi yaliyompa ushindi mgombea mwingine wa upinzani.
-
SAUTI, Matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa Kongo DR yaibua hali mseto kati ya Wakongomani, Fayulu kwenda mahakamani
Jan 10, 2019 13:47Kumekuwa na hali mseto baada ya Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kumtangaza Felix Tshisekedi wa upinzani kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliopita.
-
Chama tawala Kongo DR chataka kuangaliwa upya matokeo ya uchaguzi
Jan 10, 2019 12:33Baada ya kushindwa katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa rais, muungano wa chama tawala huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo umetangaza kwamba, unayo haki ya kutaka kuangaliwa upya matokeo hayo.
-
António Guterres: Wakongomani wajiepushe na machafuko katika kipindi hiki nyeti
Jan 10, 2019 12:13Kufuatia kutolewa matokeo ya mwanzo ya uchaguzi wa rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres amezitaka pande mbalimbali kujiepusha na vitendo vya utumiaji mabavu.
-
Tume ya Uchaguzi ya Kongo yamtangaza mgombea wa upinzani mshindi wa kiti cha urais
Jan 09, 2019 23:58Felix Tshisekedi mgombea wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliokuwa na mchuano mkali uliofanyika nchini humo Jumapili iliyopita.
-
Afrika Kusini, Zambia zaitaka Tume ya Uchaguzi Kongo itangaze matokeo ya urais
Jan 09, 2019 13:31Marais wa Afrika Kusini na Zambia wameitaka tume ya uchaguzi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutangaza matokeo ya uchaguzi wa rais ili kuondoa taharuki na wasiwasi wa kuibuka ghasia za baada ya uchaguzi katika nchi hiyo ya katikati mwa Afrika.
-
Mashauriano ya mgombea wa upinzani Kongo na kambi ya Kabila kuhusu kukabidhi madaraka kwa amani
Jan 09, 2019 03:47Wawakilishi wa Felix Tshisekedi mgombea mkuu wa kiti cha urais katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamekutana na kambi ya Rais Joseph Kabila ili kuhakikisha zoezi la kukabidhi madaraka linafanyika kwa njia ya amani nchini humo. Hayo yameelezwa na timu ya kampeni ya Tshisekedi.