Ajali ya treni yaua na kujeruhi zaidi ya watu 130 DRC
Mar 19, 2019 02:30 UTC
Ajali ya garimoshi la kusafirishia mizigo iliyotokea siku ya Jumapili katika mkoa wa Kasai wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesababisha kupoteza maisha zaidi ya watu 50 na kujeruhiwa wengine wapatao 80.
Mabehewa na garimoshi na reli zinazopita garimoshi hizo zimechakaa mno huko DRC kwani ni zile zile za tangu enzi za ukoloni, kabla ya kupata uhuru nchi hiyo tajiri kwa maliasili ya katikati mwa Afrika.
Hali ya usafiri katika nchi hiyo kiujumla ni mbaya mno kiasi kwamba wananchi wanalazimika kudandia hata magarimoshi mabovu na yaliyochakaa ya mizigo ili kufika wanakokwenda.
Mwandishi wetu Mossi Mwasi ametutayarishia ripoti kuhusu ajali hiyo.
Tags