-
Jeshi Kenya laua waandamanaji watatu, magari kadhaa yachomwa, Raila arejea nchini
Nov 17, 2017 13:20Watu watatu wameuawa hii leo wakati jeshi la polisi la Kenya lilipojaribu kutawanya waandamanaji waliokusanyika kupokea msafara wa kiongozi wa upinzani, Raila Odinga aliyerejea nchini mapema leo akitokea nje ya nchi.
-
Mahakama ya Juu ya Kenya kusikiliza kesi ya kupinga uchaguzi wa marudio wa rais
Nov 14, 2017 12:57Mahakama ya Juu ya Kenya leo imeanza kuchunguza kesi za kupinga uchaguzi wa marudio wa rais uliofanyika mwezi uliopita wa Oktoba ambapo Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta alipata ushindi wa kishindo kufuatia kujiondoa mpinzani wake mkuu Raila Odinga kwenye kinyang'anyiro hicho.
-
Ulimwengu wa Spoti, Nov 13
Nov 13, 2017 04:01Hujambo mpenzi msikilizaji wa RT na hususan ashiki wa spoti na karibu tutupie jicho matukio mawili matatu ya michezo yaliyogonga vichwa vya habari ndani na nje ya nchi katika kipindi cha siku saba zilizopita, karibu..
-
WHO yatahadharisha kuhusu ugonjwa wa virusi vya Marburg Kenya na Uganda
Nov 11, 2017 12:23Shirika la Afya Duniani (WHO) limewatahadharisha wageni wanaotembelea Hifadhi ya Taifa ya Mt Elgon juu ya hatari ya kupatwa na ugonjwa wa virusi vya Marburg.
-
Kenya yapinga hatua ya Tanzania kupiga mnada zaidi ya Ng’ombe 1,300
Nov 08, 2017 12:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Amina Mohamed ameilalamikia serikali ya Tanzania kufuatia hatua ya taifa hilo kuwapiga mnada zaidi ya ng’ombe 1,300 walioingia nchini humo kinyume na sheria.
-
Usafiri wasitishwa Mandera, Kenya baada ya hujuma ya magaidi wa Al Shabab
Nov 07, 2017 10:54Hujuma ya kundi la kigaidi la Al Shabab katika Kaunti ya Mandera, kaskazini mashariki mwa Kenya imepelekea usafiri kusitishwa kwa muda wa siku tatu.
-
Eneo la Pwani latoa wito wa kujitenga na ardhi ya Kenya
Nov 03, 2017 23:50Viongozi wa eneo la Pwani nchini Kenya wametoa mwito wa kutaka kujitenga eneo hilo na ardhi ya nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
-
Rais wa Zambia awaonya majaji wasifuate mkondo wa wenzao wa Kenya
Nov 03, 2017 11:01Rais Edgar Lungu wa Zambia ametoa tahadhari kwa majaji wa nchi hiyo dhidi ya kufuata mkondo wa majaji wa Kenya wa kumzuia kugombea urais katika uchaguzi ujao nchini humo.
-
'Polisi Kenya wameshaua watu 36 katika machafuko ya uchaguzi'
Nov 01, 2017 12:47Shirika moja la haki za binadamu la Kenya limetoa ripoti na kusema kuwa, zaidi ya watu 36 wameshauliwa na polisi tangu tarehe 11 Agosti siku yalipotangazwa matokeo ya uchaguzi wa kwanza wa rais nchini Kenya hadi hivi sasa.
-
Majaji wa Mahakama ya Kilele ya Kenya wanyimwa ulinzi wa ziada
Nov 01, 2017 04:35Serikali ya Kenya imekataa ombi lililowasilishwa na majaji wa Mahakama ya Kilele ya nchi hiyo wakitaka kupatiwa ulinzi wa ziada baada ya mmoja wa walinzi wao kupigwa risasi na hivyo kuwazuia kusikiliza kesi ililiyowasilishwa mahakamani na wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu ambayo ingepelekea kuakhirishwa uchaguzi wa marudio wa urais wa wiki iliyopita.