-
HRW, AI: Polisi ya Kenya imeua watu zaidi ya 67 katika maandamano
Oct 16, 2017 04:47Mashirika ya kutetea haki za binadamu ya Human Rights Watch na Amnesty International yamesema polisi ya Kenya imeua watu wasiopungua 50 katika maandamano ya upinzani ya kushinikiza mabadiliko kwenye Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC, kuelekea uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26.
-
Ulimwengu wa Michezo
Oct 16, 2017 04:38Hujambo mpenzi mwanaspoti na karibu katika dakika hizi chache za kukupasha matukio mawili matatu yaliyotikisa uga wa michezo duniani, ndani ya siku saba zilizopita. Usibanduke kando ya radio yako hadi tamati ya kipindi, karibu……...
-
Askofu asilimu Kenya na wafuasi wake, ageuza kanisa lake kuwa msikiti
Oct 15, 2017 23:03Askofu mmoja nchini Kenya amesilimu akiwa na wafuasi wake na kulibadilisha kanisa lake kuwa msikiti.
-
Wapinzani Kenya waendeleza maandamano ya kutaka mabadiliko katika tume ya uchaguzi
Oct 15, 2017 11:32Muungano mkuu wa upinzani Kenya, NASA, leo umeendeleza maandamano ya kutaka mabadiliko katika Tume Huru ya Uchaguzi IEBC.
-
Wanafunzi 6 na mlinzi wauawa baada ya shule kuvamiwa na maharamia Kenya
Oct 14, 2017 06:06Kwa akali wanafunzi sita na bawabu wa shule moja katika mji wa Lokichogio, kaskazini mwa Kenya wameuawa baada ya shule yao kuvamiwa na maharamia wanaoaminika kutoka Sudan Kusini, usiku wa kuamkia leo.
-
Watu 3 wauawa katika maandamano ya wapinzani nchini Kenya
Oct 13, 2017 11:29Watu watatu wameripotiwa kuuawa katika maandamano ya wapinzani nchini Kenya ambao wanataka mabadiliko katika Tume Huru ya Uchaguzi IEBC.
-
Mwangwi wa hatua ya kinara wa chama kikuu cha upinzani Kenya kujiondoa katika uchaguzi wa Rais
Oct 11, 2017 07:24Kiongozi wa muungano wa upinzani wa National Super Alliance (NASA) nchini Kenya ametangaza kuwa, hatagombea katika uchaguzi wa marudio wa rais ambao umepangwa kufanyika tarehe 26 Oktoba akisema kwamba uchaguzi huo hautakuwa huru na wa haki.
-
Odinga ajitoa kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa marudio wa rais wa Kenya
Oct 10, 2017 13:21Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga ametangaza leo kuwa hatogombea katika uchaguzi wa marudio wa rais ulioamriwa kuitishwa tena na Mahakama ya Juu ya nchi hiyo ambao umepangwa kufanyika tarehe 26 Oktoba akisema kwamba uchaguzi huo hautokuwa huru na wa haki.
-
Watu wenye silaha wawafyatulia risasi waandamanaji jijini Nairobi, Kenya
Oct 09, 2017 11:25Habari kutoka Kenya zinaarifu kwamba watu wenye silaha wamefyatua risasi dhidi ya mamia ya waandamanaji wa upinzani waliokuwa wanaelekea zilipo ofisi za Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) jijini Nairobi, mji mkuu wa Kenya.
-
Polisi ya Kenya yatumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa NASA
Oct 06, 2017 11:39Polisi nchini Kenya wamelazimika kutumia mabomu ya gesi ya kutoa machozi kuwatawanya wafuasi wa muungano wa upinzani NASA walioandamana katika miji ya Nairobi na Kisumu kushinikiza mabadiliko katika Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka IEBC.