-
Vita vya Libya vimesababisha watu 268,000 kuwa wakimbizi
Aug 30, 2019 03:37Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Libya vimepelekea zaidi ya watu 268,000 kuwa wakimbizi.
-
Baada ya kudukuliwa mtandao wake, serikali ya Libya yakanusha kuvunjwa
Aug 29, 2019 12:13Duru moja ya Baraza la Uongozi la Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya inayotambulika kimataifa na ambayo inaongozwa na Fayez al Sarraj imekanusha madai kwamba imevunjwa na mawaziri wake wote kujiuzulu.
-
Mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Libya wakutana Japan pembizoni mwa kikao cha TICAD
Aug 28, 2019 07:17Mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Libya wamekutana nchini Japan na kujadili matukio ya hivi karibuni nchini Libya na eneo zima la Afrika Kaskazini.
-
Serikali ya Libya yaituhumu UAE kuwa imeshambulia Tripoli kwa mabomu
Aug 26, 2019 01:39Serikali ya Mapatano ya Kitaifa Libya (GNA) inayoongozwa na Waziri MKuu Fayez al-Sarraj imesema ndege za kivita za Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) zimehusika katika kudondosha mabomu katika mji mkuu, Tripoli.
-
Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa Libya yafichua: Kikosi cha jeshi la Ufaransa kinamsaidia Haftar
Aug 23, 2019 02:31Maafisa wa Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya wamefichua kuwa kundi moja la jeshi la Ufaransa linalomsaidia jenerali mstaafu Khalifa Haftar limewajengea wapiganaji wa kiongozi huyo muasi kituo cha kurushia ndege zisizo na rubani katika bandari ya mafuta ya al Sidr huko kaskazini mwa Libya.
-
Gadi ya pwani ya Libya yaokoa wahajiri 37
Aug 20, 2019 13:14Gadi ya Pwani ya Libya imetangaza kuwaokoa wahajiri haramu wapatao 37 katika pwani ya Khoms. Taarifa ya Jeshi la Majini la Libya imesema wahajiri hao walikuwa ni kutoka nchi 7 za Kiarabu na Kiafrika.
-
Mapigano yaendelea Libya; mji wa Misrata washambuliwa mara 13
Aug 19, 2019 03:01Ndege za kivita za kundi la wanamgambo kwa jina la Jeshi la Kitaifa la Libya linaloongozwa na Jenerali Khalifa Haftar zimeushambulia mji wa Misrara mara 13.
-
UN yalaani mashambulizi dhidi ya vifaa na wafanyakazi wa afya Tripoli
Aug 16, 2019 08:06Umoja wa Mataifa umelaani hujuma dhidi ya vifaa na wafanyakazi wa huduma za afya katika mji mkuu wa Libya, Tripoli.
-
Jenerali Haftar apinga kuongezwa muda wa usitishaji mapigano Tripoli
Aug 15, 2019 07:24Kamanda wa kundi la wanamgambo wanaojiita jeshi la kitaifa la Libya amepinga kuongezwa muda wa kusimamisha mapigano nchini humo na kutangaza kuanza tena mashambulizi.
-
Rais wa Afrika Kusini kuwasili nchini Tanzania kesho Jumatano
Aug 13, 2019 02:31Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini kesho Jumatano anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku mbili pamoja na kuhudhuria Mkutano Mkuu wa 39 wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC.