-
Walibya waandamana mjini Tripoli kuulaani utawala wa Saudi Arabia
May 04, 2019 09:22Raia wa Libya wamefanya maandamano mbele ya ubalozi wa Saudi Arabia mjini Tripoli, wakilaani uingiliaji haribifu wa Riyadh katika masuala ya ndani ya nchi yao.
-
Maandamano ya wananchi yaendelea Algeria kupinga serikali ya mpito
May 04, 2019 03:43Wananchi wa Algeria wameendelea na maandamano yao ya kupinga serikali ya mpito ya nchi hiyo na kuishutumu kuwa inapoteza muda.
-
Walibya waandamana mjini Tripoli kulaani hatua za Ufaransa dhidi ya nchi yao
Apr 27, 2019 08:28Raia wa Libya wamefanya maandamano katika medani kuu ya mji wa Tripoli wakiwa wamevalia vizibao vya njano kama wanavyofanya washiriki wa maandamano ya vizibao vya njazo kupinga siasa za kiuchumi za serikali ya Ufaransa, ambapo nao wamelaani mienendo hasi ya serikali ya Paris dhidi ya nchi yao.
-
Wanaharakati waandamana London, Uingereza kulaani ukatili wa Saudia
Apr 27, 2019 03:18Kwa mara ya pili ndani ya wiki moja, wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu wamefanya maandamano nje ya ubalozi wa Saudi Arabia katika mji mkuu wa Uingereza, London kulaani ukatili wa hivi karibuni wa watawala wa Aal-Saud dhidi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia.
-
Waandamanaji Algeria wataka kupandishwa kizimbani ndugu ya Bouteflika
Apr 26, 2019 22:11Wananchi wa Algeria jana waliandamana tena ikiwa ni Ijumaa ya 10 mtawalia ya maandamano yao ambapo mbali na kusisitiza juu ya kuachia ngazi viongozi na maafisa wote wa serikali waliokuwa katika kipindi cha utawala wa Abdelaziz Bouteflika, Rais wa nchi hiyo aliyelazimika kujiuzulu, wametoa mwito wa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria Said Bouteflika, ndugu ya rais huyo mkongwe aliyejiuzulu kufuatia maandamano ya wananchi.
-
Wasudan waendeleza maandamano ya kushinikiza utawala wa kiraia
Apr 26, 2019 09:52Maelfu ya wananchi wa Sudan wamesali Sala ya Ijumaa nje ya makao makuu ya jeshi la nchi hiyo mjini Khartoum, siku moja baada ya maandamano makubwa kushuhudiwa katika kona mbalimbali za mji mkuu huo, kulishinikiza jeshi likabidhi madaraka kwa raia.
-
Raia wa Italia waandamana kuupinga utawala wa Kizayuni Israel na kuiunga mkono Palestina
Apr 26, 2019 03:31Sambamba na kusherehekea mwaka wa 74 wa kuwa huru nchi ya Italia na utawala wa Kifashisti, raia wa nchi hiyo mjini Roma, mji mkuu wa Italia wamefanya maandamano kuliunga mkono taifa madhlumu la Palestina.
-
Wakuu wa Baraza la Mpito la Kijeshi la Sudan wajiuzulu
Apr 25, 2019 03:17Viongozi watatu kati ya 10 wa Baraza la Mpito la Kijeshi la Sudan wametangaza kujiuzulu, huku wananchi wa nchi hiyo wakitazamiwa kuendelea na maandamano yao leo Alkhamisi, kulishinikiza jeshi likabidhi madaraka kwa raia.
-
Waandamanaji Sudan kutangaza Baraza la Mpito la Kiraia
Apr 21, 2019 09:45Chama cha Wanataaluma Sudan kimetangaza kuwa kinajiandaa kutangaza Baraza la Mpito la Kiraia, litakalochukua madaraka kutokana kwa Baraza la Mpito la Kijeshi la nchi hiyo.
-
Walibya waandamana kulaani hatua ya Trump kumpigia simu Jenerali Haftar
Apr 20, 2019 08:37Wananchi wa Libya wamefanya maandamano mjini Tripoli kukosoa hatua ya Rais Donald Trump kumpigia simu jenerali muasi Khalifa Haftar mwenye makao yake katika mji wa Benghazi, magharibi mwa Libya, na ambaye amekuwa akiendesha kampeni ya kijeshi ya kutaka kuuteka mji mkuu Tripoli.