-
Tunisia yaanza kusikiliza kesi ya mauaji ya dikteta wa zamani wa nchi hiyo
Jul 14, 2018 03:32Serikali ya Tunisia imeanza kusikiliza kesi dhidi ya dikteta wa zamani wa nchi hiyo, Zine El Abidine Ben Ali, kwa kuhusika na mauaji ya waandamanaji katika vuguvugu lililomuondoa madarakani mwaka 2011.
-
Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan miaka 10 jela kwa ufisadi
Jul 06, 2018 09:55Mahakama ya Kupambana na Ufisadi ya Pakistan imempata na hatia ya ufisadi wa kifedha aliyekuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo pamoja na binti yake na kuwahukumu kifungo cha miaka 10 jela.
-
Utawala wa Bahrain wawahukumu kifo wanazuoni watatu wa Kiislamu
Jun 17, 2018 10:13Mahakama ya utawala wa Aal-Khalifa nchini Bahrain imetoa hukumu ya adhabu ya kifo dhidi ya wanazuoni watatu wa Waislamu wa madhehebu ya Shia wa nchi hiyo kwa tuhuma bandia dhidi yao, ikiwa ni muendelezo wa hukumu zisizo za kiuadilifu zinazotolewa na watawala madikteta wa nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi.
-
Mahakama yatupilia mbali kesi ya upinzani kuhusu kura ya maoni Burundi
May 31, 2018 10:28Mahakama ya Katiba ya Burundi imetupilia mbali kesi iliyowasilisha na muungano wa upinzani nchini humo kupinga matokeo ya kura ya maoni ya kuifanyia marekebisho katiba ya nchi, yaliyoipa ushindi kambi ya serikali.
-
Mahakama ya Katiba Madagascar yaagiza kuundwa serikali ya muungano
May 26, 2018 03:29Mahakama ya Katiba nchini Madagascar imemuagiza Rais Hery Rajaonarimampianina wa nchi hiyo kuvunja serikali ya sasa na kuunda serikali ya muungano, kwa lengo la kutamatisha mgogoro wa kisiasa unaoshuhudiwa katika kisiwa hicho kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.
-
Upinzani Burundi waenda mahakamani kupinga matokeo ya kura ya maoni
May 25, 2018 03:04Muungano wa upinzani nchini Burundi unaoongozwa na Agathon Rwasa jana Alkhamisi ulienda mahakamani kupinga matokeo ya kura ya maoni ya kuifanyia marekebisho katiba ya nchi, yaliyoipa ushindi kambi ya serikali.
-
Amnesty: Ni upuuzi kuwavua uraia Wabahrain 115 katika 'kesi ya umati'
May 17, 2018 09:42Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limekosoa vikali hatua ya hivi karibuni ya Bahrain ya kuwafunga jela na kuwapokonya uraia makumi ya wanaharakati wa kisiasa ambao wanaonekana kuwa wakosoaji wakubwa wa utawala wa Aal-Khalifa.
-
Bahrain yawapokonya uraia wapinzani 115, yawafunga jela maisha 53 miongoni mwao
May 15, 2018 09:27Katika kile kinachoonekana ni muendelezo wa ukandamizaji na mbinyo dhidi ya wapinzani na wakosoaji wa serikali, utawala wa Aal-Khalifa umewavua uraia wananchi 115 wa Bahrain, huku ukiwahukumu kifungo cha maisha jela 53 miongoni mwao.
-
Kuna uwezekano wa Trump kufikishwa mahakamani ili kusailiwa
May 02, 2018 03:14Gazeti la Washington Post linalochapishwa nchini Marekani limeandika kuwa kuna uwezekano rais wa nchi hiyo Donald Trump akatakiwa afike mahakamani ili kusailiwa kuhusiana na kadhia ya kuingilia Russia mchakato wa uchaguzi wa rais wa Marekani wa mwaka 2016.
-
Mahakama yamuuzulu Waziri Mkuu na kuvunja Bunge Gabon
May 01, 2018 09:59Mahakama ya Katiba nchini Gabon imeagiza kuvunjwa kwa Bunge la Taifa la nchi hiyo sanjari na kumuuzulu Waziri Mkuu wa nchi hiyo, hatua ambayo imesitisha shughuli za serikali ya Rais Ali Bongo wa nchi hiyo.