-
Zarif: Wamarekani wametengwa katika siasa za kimataifa
Jul 11, 2019 07:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezitaja siasa na machaguo yasiyofaa ya Marekani kuwa miongoni mwa sababu za ushindi wa muqawama na kutengwa Washington katika uga wa siasa za kimataifa.
-
Aoun: Kuiwekea vikwazo Hizbullah ni kuivunjia heshima Lebanon
Jul 11, 2019 06:52Rais wa Lebanon amesema kuwa vikwazo vya Marekani dhidi ya wawakilishi wa harakati ya Hizbullah ya nchi hiyo ni sawa na kuivunjia heshima Lebanon.
-
Russia: Marekani haina haki ya kuikosoa Iran kuhusiana na JCPOA
Jul 11, 2019 03:48Mwakilishi wa Russia katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia IAEA amesema kuwa Marekani haina haki yoyote ya kisheria ya kuikosoa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutokana na hatua yake ya kupunguza ahadi zake kuhusiana na mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA.
-
Sisitizo la Rais Maduro la uwezekano wa kufikiwa makubaliano na wapinzani kwa sharti Marekani iache kuingilia mambo ya Venezuela
Jul 10, 2019 03:20Kuendelea mgogoro wa kisiasa wa Venezuela na kushindwa wapinzani kuiangusha serikali ya Rais Nicolas Maduro kumemfanya Juan Guaido, kiongozi wa upinzani nchini humo akubali pendekezo la upatanishi wa Norway na kufanyika mazungumzo baina ya wapinzani na wawakilishi wa serikali ya Caracas.
-
UN yasikitishwa na hali mbaya inayowakabili wahajiri nchini Marekani
Jul 09, 2019 03:49Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa sanjari na kukosoa vikali sera za wahajiri za utawala wa Rais Donald Trump, ameeleza kusikitishwa kwake na hali mbaya inayowakabili wahajiri na wakimbizi nchini Marekani.
-
Ujerumani yakataa ombi la Marekani la kutuma askari Syria
Jul 09, 2019 03:48Rais Donald Trump wa Marekani Disemba mwaka 2018 aliwaahidi Wamarekani kwamba ataliondoa jeshi la nchi hiyo huko Syria. Trump alitoa ahadi hiyo katika kile kinachoaminika kuwa ni sehemu ya kutekeleza kampeni yakee ya kubakia ikulu ya White House.
-
Trump na balozi wa Uingereza washambuliana kwa maneno
Jul 08, 2019 03:16Rais Donald Trump amemshambulia vikali balozi wa Uingereza mjini Washington aliyemtaja kiongozi huyo wa Marekani kama mtu mtepetevu, asiye na tajriba na anayeendesha Ikulu ya White House kishaghalabaghala.
-
Iran: Ni haki yetu kuchukua hatua za kukabiliana na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani
Jul 07, 2019 22:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, ni haki ya Tehran kuchukua hatua za kisheria ndani ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA katika kukabiliana na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani dhidi yake.
-
"Siasa za Marekani dhidi ya Iran zimefeli"
Jul 07, 2019 22:12Naibu wa Mkuu wa Baraza la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, siasa za serikali ya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimefeli.
-
Hamas yaapa kudumaza mpango wa Trump wa "Muamala wa Karne"
Jul 06, 2019 21:54Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa itaendeleza harakati za kupinga mpango eti wa amani uliozusha makelele mengi wa Rais Donald Trump wa Marekani baina ya utawala haramu wa Israel na Wapalestina uliopewa jina la "Muamala wa Karne"