-
UN yakosoa ukandamizaji Misri kuelekea uchaguzi wa rais
Mar 07, 2018 22:10Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amekosoa mazingira ya vitisho, ukandamizaji na kuwekewa mbinyo wanasiasa wa upinzani nchini Misri kuelekea uchaguzi wa rais unaotazamiwa kufanyika baadaye mwezi huu.
-
Bahram Qassemi ajibu tuhuma za Saudia na Misri dhidi ya Iran
Mar 07, 2018 11:47Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Bahram Qassemi sambamba na kutupilia mbali tuhuma za kujikariri dhidi ya taifa hili zilizotolewa katika ripoti ya pamoja ya Saudia na Misri, amesema kuwa tuhuma hizo hazina msingi, ni za kubuni na ni makosa haribifu ya kukaririwa.
-
Kundi moja la kigaidi lasambaratishwa nchini Misri
Mar 04, 2018 13:36Duru za usalama za nchini Misri zimetangaza habari ya kusambaratishwa kundi moja la kigaidi lenye mfungamano na Daesh (ISIS) katika mkoa wa Minya, kusini mwa mji mkuu Cairo.
-
Mahakama Misri yaidhinisha Saudia kupewa visiwa vya nchi hiyo
Mar 04, 2018 04:25Mahakama ya Juu nchini Misri imefutilia mbali maamuzi yaliyotolewa na mahakama za chini za nchi hiyo kuhusu mpango wa kukabidhi visiwa viwili vya kistratajia vya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kwa Saudi Arabia.
-
Magaidi 13 wengine waangamizwa Sinai Misri
Mar 01, 2018 12:01Jeshi la Misri limetangaza habari ya kuangamizwa magaidi 13 katika muendelezo wa operesheni za wanajeshi wa nchi hiyo katika Rasi ya Sinai.
-
Mwendesha mashtaka wa Misri ataka kufuatiliwa vyombo vya habari nchini humo
Feb 28, 2018 13:01Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Misri ametaka kufuatiliwa kwa kina na kwa karibu shughuli za vyombo vya habari na kuchukuliwa hatua za kisheria dhidi ya chombo chochote cha habari ambacho kinavuruga usalama na kuhatarisha maslahi ya taifa.
-
HRW yaikosoa serikali ya Misri kwa ukandamizaji
Feb 26, 2018 23:21Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeikosoa serikali ya Misri kwa hatua yake ya kuwatia mbaroni kiholela wanasiasa wa upinzani nchini humo.
-
Misri yazidi kukandamiza wapinzani, mali za mkuu wa chama cha Misri Imara zazuiwa
Feb 26, 2018 03:59Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa serikali ya Misri imetoa amri ya kuzuiliwa mali zote za mkuu wa chama cha Misri Imara ambaye alitiwa mbaroni hivi karibuni baada ya kumkosoa Rais Abdel Fattah el Sisi wa nchi hiyo.
-
Kampeni za uchaguzi wa rais Misri zaanza
Feb 25, 2018 03:58Kamepeni za uchaguzi wa Rais Misri zilianza Jumamosi huku Rais Abdel Fattah el-Sisi akitazamiwa kupata ushindi kwa urahisi baada ya wapinzani wake asili kukamatwa, kufungwa jela au kutishwa na hivyo kujiondoa katika mchuano huo.
-
Jumamosi, 24 Februari, 2018
Feb 23, 2018 21:16Leo ni Jumamosi tarehe 7 Mfunguo Tisa Jamadi Thani 1439 Hijria mwafaka na tarehe 24 Februari 2018 Miladia.