-
Msumbuji yachukua uwenyekiti wa SADC
Aug 18, 2020 03:37Tanzania imekabidhi Msumbiji uwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika, SADC huku jumuiya hiyo ikiadhimisha miaka 40 tangu kuasisiwa kwake.
-
Kampuni ya Msumbiji: Shehena ya ammonium nitrate iliyosababisha mlipuko Beirut ilikuwa mali yatu
Aug 08, 2020 13:36Kampuni moja ya kutengeneza baruti ya Msumbiji imetangaza kuwa, shehena ya mzigo iliyokuwa imesimamishwa katika bandari ya Beirut ambayo imesababisha mlipuko wa tarehe 4 Agosti ilikuwa mali ya kampuni hiyo.
-
Maafisa usalama wa Msumbiji waua magaidi 50 Cabo Delgado
May 15, 2020 12:26Waziri wa Mambo ya Ndani wa Msumbiji amesema maafisa usalama wa nchi hiyo wamefanikiwa kuwaangamiza magaidi 50 ndani ya siku chache zilizopita katika eneo la kaskazini la Cabo Delgado.
-
Magaidi 129 wameuawa ndani ya mwezi mmoja na maafisa usalama Msumbiji
Apr 29, 2020 11:12Waziri wa Mambo ya Ndani wa Msumbiji ametangaza habari ya kuuawa makumi ya wanachama wa magenge ya kigaidi kaskazini mwa nchi katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
-
Makumi ya wanakijiji wauawa na magaidi kaskazini mwa Msumbiji
Apr 22, 2020 12:57Jeshi la Polisi la Msumbiji limetangaza habari ya kuuawa makumi ya watu katika shambulizi jipya la kigaidi lililotokea huko kaskazini mwa nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.
-
Kampuni ya Total ya Ufaransa inatuhumiwa kueneza virusi vya Corona nchini Msumbiji
Apr 18, 2020 00:42Maafisa Afya wa Msumbiji wamesema kuwa kampuni ya mafuta ya Total ya Ufaransa imehusika kueneza maambukizi ya virusi vya corona nchini humo.
-
"Wahajiri" 60 wapatikana wameaga dunia ndani ya lori Msumbiji
Mar 26, 2020 11:27Miili zaidi ya 60 imepatikana ndani ya lori la mizigo katika mkoa wa Tete, kaskazini magharibi mwa Msumbiji.
-
UN: Vijiji vinachomwa na watu wanakatwa vichwa na kutekwa nyara kwa halaiki kaskazini mwa Msumbiji
Feb 08, 2020 12:57Umoja wa Mataifa umesema, watu wanayakimbia makazi yao ili kujinusuru na wimbi la hujuma na mashambulio katika mkoa wa Cabo Delgado, kaskazini mwa Msumbiji ambako mashuhuda wamesema, raia wanakatwa vichwa na kutekwa nyara kwa umati huku vijiji vya eneo hilo vikiteketezwa kwa moto.
-
Rais Nyusi wa Msumbiji aapishwa, upinzani wasusia
Jan 16, 2020 02:32Rais Filipe Nyusi wa Msumbiji alikula kiapo cha kulitumikia taifa jana Jumatano katika hafla iliyosusiwa na viongozi mashuhuri wa upinzani nchini humo, wanaosisitiza kuwa kuliwepo na udanganyifu katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka uliomalizika wa 2019.
-
Mahakama Msumbiji yapinga rufaa ya wapinzani kuhusu matokeo ya uchaguzi
Nov 15, 2019 13:51Mahakama ya Katiba Msumbiji imetupilia mbali rufaa ya chama cha upinzani cha Renamo ambacho kilikuwa kinataka kufutwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa hivi karibuni.