-
Nchi za Kiislamu zaafiki mpango wa UN wa kuwasaidia Waislamu Myanmar
Sep 10, 2017 14:25Nchi za Kiislamu duniani zimeafiki mpango wa Umoja wa Mataifa wa kuwasaidia wakimbizi 300,000 Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar ambao wamekimbilia nchini jirani ya Bangladesh kuokoa maisha yao.
-
Marekani kuimarisha ushirikiano wa kijeshi na Myanmar inayoua Waislamu
Sep 10, 2017 07:15Katika hali ambayo jamii ya kimataifa inaendelea kulaani na kukosoa vikali mauaji na ukatili wanaofanyiwa Waislamu wa kabila la Rohingya katika jimbo la Rakhine nchini Myanmar, Marekani ipo mbioni kuimarisha ushirikiano wake wa kijeshi na nchi hiyo ya kusini mashariki mwa Asia.
-
Zarif: Viongozi wa nchi za Kiislamu watazungumzia jinai dhidi ya Waislamu wa Myanamr
Sep 10, 2017 02:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema viongozi wa nchi za Kiislamu wanaokutana katika kikao cha Sayansi na Teknolojia nchini Kazakhstan watazungumzia pia jinai zinazoendelea kufanywa dhidi ya Waislamu wa Myanmar.
-
UN yaeleza wasi wasi wake kuhusu wimbi la wakimbizi wa Rohingya nchini Bangladesh
Sep 09, 2017 07:45Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limeeleza wasi wasi mkubwa lilionao kutokana na kuendelea kumiminika idadi kubwa ya wakimbizi Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Bangladesh.
-
Desmond Tutu amtaka San Suu Kyi kukomesha mauaji ya Waislamu Myanmar
Sep 09, 2017 04:31Askofu Mkuu wa Afrika Kusini, Desmond Tutu amemtaka Mshauri Mkuu wa Serikali ya Myanmar na mshindi mwenzake wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Aung San Suu Kyi kukomesha mauaji yanayofanywa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya.
-
Zarif autaka Umoja wa Mataifa kusitisha mauaji ya Waislamu Myanmar
Sep 09, 2017 04:31Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za kusitisha ukatili unaofanyika kwa mpangilio maalumu dhidi ya Waislamu nchini Myanmar.
-
Ayatullah Movahhedi Kermani: Mataifa ya Kiislamu yaamke dhidi ya jinai za Mabudha wa Myanmar
Sep 08, 2017 18:54Hatibu wa Swala ya Ijumaa hapa Tehran amesema kuwa hakuna matumaini ya kuona taasisi za kimataifa zikisaidia kuzuia mauaji ya Waislamu wa Rohingya nchini Myanmar na ameyataka mataifa ya Kiislamu kuamka na kusimama kidete dhidi ya jinai zinazofanywa na jeshi na Mabudha wa nchi hiyo.
-
Mauaji ya kimbari ya Waislamu wa Myanmar
Sep 08, 2017 17:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekemea tena mauaji ya kimbari yanayofanyika nchini Myanmar dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya na kusema kuwa: Jamii ya Kimataifa inapaswa kuchukua hatua haraka bila ya kucheleza zaidi.
-
Wairani waandamana kupinga mauaji ya Waislamu nchini Myanmar
Sep 08, 2017 17:05maelfu ya Wairani waliohudhuria ibada ya Swala ya Ijumaa kote hapa nchini leo wamefanya maandamo katika miji mbalimbali wakipinga na kulaani mauaji yanayoendelea kufanywa na jeshi na Mabudha wa Myanmar dhidi ya Waislamu nchini humo.
-
Mauaji ya Waislamu wa Rohingya ni njama iliyoratibiwa
Sep 08, 2017 07:01Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH) limetoa taarifa na kusema kuwa, mauaji ya hivi sasa ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar na hatua ya mashirika ya kutetea haki za binadamu ya kupuuza ukatili huo ni jambo linaloashiria njama iliyoratibiwa tangu zamani dhidi ya Waislamu.