-
Iran: Jamii ya kimataifa ikomeshe mauaji ya Waislamu wa Myanmar
Sep 08, 2017 04:30Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua za kivitendo za kukomesha uangamizaji wa kizazi wanayofanyiwa Waislamu wa kabila la Rohingya na mabudha wa Myanmar.
-
Hilali Nyekundu ya Iran kutuma misaada kwa Waislamu wa Rohingya
Sep 07, 2017 14:33Shirika la Hilali Nyekundu la Jamhuri ya Kiislamau ya Iran limesema limeandaa misaada ya kibinadamu kwa ajili ya Waislamu wa kabila la Rohingya nchini Myanmar.
-
Jitihada za serikali ya Bangladesh za kuwahamishia wakimbizi wa Rohingya katika kisiwa cha mbali
Sep 07, 2017 08:07Baada ya kushadidi vitendo vya ukatili na mauaji dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya wa Myanmar na kulazimika maelfu miongoni mwao kuwa wakimbizi, serikali ya Bangladesh imetangaza kwamba, inakusudia kuwahamishia wakimbizi hao Waislamu katika kisiwa kimoja cha nchi hiyo katika Ghuba ya Bengal na hivyo kuwapatia makazi ya muda huko.
-
Waislamu 300,000 watazamiwa kukimbia mauaji nchini Myanmar
Sep 07, 2017 07:41Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuwa Waislamu zaidi ya 300,000 wanatazamiwa kukimbia mauaji na dhulma wanazotendewa nchini Myanmar na kuelekea katika nchi jirani ya Bangladesh.
-
Iran: Mataifa yote yanapaswa kuzuia kutokea maafa ya kibinadamu Myanmar
Sep 07, 2017 04:38Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameelezea wasiwasi mkubwa alionao kutokana na hali mbaya na ya kusikitisha wanayokabiliwa nayo Waislamu wa Myanmar na kuelezea juu ya kuundwa kundi ma mawasiliano la nchi za Kiislamu katika siku za usoni.
-
Larijani: Tume ya kutafuta ukweli ya UN ichunguze hali ya Myanmar
Sep 07, 2017 04:21Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amelaani mauaji ya Waislamu wa Myanmar na kutaka ujumbe wa kutafuta ukweli wa Umoja wa Mataifa utumwe haraka nchini humo kuchunguza hali ya mambo na utumaji misaada ya kibinadamu.
-
ISESCO yataka Aung San Suu Kyi anyang'anywe tuzo ya Nobel, Waislamu waendelea kuuawa Myanmar
Sep 06, 2017 12:12Shirika la Elimu, Sayansi na Utamasdu la Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (ISESCO) limetangaza kuwa, Mshauri Mkuu wa Serikali ya Myanmar, Aung San Suu Kyi anapaswa kunyang'anywa Tuzo ya Amani ya Nobel kutokana na mauaji ya kutisha yanayoendelea kufanyika nchini humo dhidi ya Waislamu.
-
Myanmar yatega mabomu ardhini katika mpaka na Bangladesh kuwazuia Waislamu kuondoka
Sep 06, 2017 07:57Inaarifiwa kuwa serikali ya Myanmar inatega mabomu ya ardhini katika mpaka wa nchi hiyo na Bangladesh ili kuwazuia Waislamu wa kabila la Rohingya kuondoka nchini humo.
-
BHRN: Sio Waislamu wa Rakhine tu wanaouawa Myanmar
Sep 06, 2017 03:49Shirika moja la kutetea haki za binadamu nchini Myanmar limetoa ripoti iliyofichua kuwa Waislamu katika maeneo yote ya nchi hiyo wanauawa na kuhujumiwa na wanajeshi wa nchi hiyo na sio wa kabila la Rohingya tu katika mkoa wa Rakhine.
-
Kuendelea jinai dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini Myanmar
Sep 05, 2017 02:34Idadi kadhaa ya Waislamu wa jamii ya Rohingya wamefariki dunia katika Mto Naf katika mpaka wa Myanmar na Bangladesh walipokuwa wakikimbia ukandamizaji unaofanywa na wanajeshi wa serikali ya nchi hiyo dhidi ya jamii hiyo.