-
Polisi wa Niger wanaendelea kuzingira ubalozi wa Ufaransa
Sep 01, 2023 23:14Polisi nchini Niger wanaendelea kuzingira majengo ya ubalozi wa Ufaransa mjini Niamey, huku Baraza la Kijeshi linalotawala nchi hiyo likichukua uamuzi wa kupiga marufuku shughuli za mashirika ya kimataifa na yasiyo ya kiserikali.
-
Tarehe ya mwisho iliyotolewa na Niger kwa askari wa Ufaransa kuondoka katika ardhi ya nchi hiyo
Aug 31, 2023 23:33Baraza la Taifa kwa ajili ya Ulinzi wa Wat'ani, (National Council for the Safeguard of the Homeland, CNSP) ambalo liliundwa hivi majuzi na viongozi wa mapinduzi ya kijeshi nchini Niger, limeitaka Ufaransa ihakikishe kuwa ifikapo Septemba 3, iwe imeshaondoa vikosi vya jeshi lake vilivyoko nchini humo.
-
Niger yawataka wanajeshi wa mkoloni Ufaransa waondoke nchini humo haraka
Aug 31, 2023 03:23Serikali ya Niger imetoa amri kwa wanajeshi wa mkoloni kizee wa Ulaya yaani Ufaransa wafungashe virago na toke nchini humo haraka.
-
Nigeria yaahidi kupunguza vikwazo vya ECOWAS dhidi ya Niger
Aug 30, 2023 09:54Msemaji wa ofisi ya rais wa Nigeria amesema nchi hiyo pamoja na Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi, ECOWAS zitapunguza baadhi ya vikwazo zilivyoiwekea Niger.
-
Kiongozi wa mapinduzi Niger: Niko tayari kumwachia huru Bazoum
Aug 24, 2023 23:38Kiongozi wa mapinduzi nchini Niger, Jenerali Abdourahamane Tiani, amekutana na ujumbe wa wanazuoni wa Kiislamu wa Nigeria, huku mashinikizo za kikanda na kimataifa yakiongezeka dhidi ya utawala wa kijeshi wa Niamey kwa shabaha ya kurejesha utawala wa kikatiba.
-
Umoja wa Afrika (AU) waisimamishia uanachama Niger
Aug 22, 2023 23:09Umoja wa Afrika (AU) umesimamisha uanachama wa Niger katika taasisi hiyo kubwa zaidi ya kibara; huo ukiwa ni muendelezo wa vikwazo na mashinikizo dhidi ya nchi hiyo ya Afrika Magharibi kufuatia mapinduzi ya kijeshi ya mwezi uliopita.
-
Uwezekano wa shambulio la kijeshi dhidi ya Niger wazidi kupata nguvu
Aug 20, 2023 07:43Huku mzozo wa kisiasa nchini Niger ukiendelea, ECOWAS (Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi) imeamua kufanya shambulio la kijeshi dhidi ya nchi hiyo, lakini haijatangaza tarehe ya kuanza shambulio hilo.
-
Kiongozi wa mapinduzi Niger: Tuko tayari kwa mazungumzo, na vita ikilazimu
Aug 20, 2023 03:23Kiongozi wa mapinduzi yaliyomuondoa madarakani Rais Mohammed Bazoum wa Niger amesema yupo tayari kufanya mazungumzo ili kuepusha mgogoro na mapigano baina ya nchi hiyo na Jumuiya Kiuchumi ya Magharibi mwa Afrika (ECOWAS) lakini anasisitiza kuwa, taifa hilo limejiandaa kujihami.
-
Taharuki yatanda nchini Niger baada ya ECOWAS kuamua tarehe ya kuishambulia nchi hiyo
Aug 19, 2023 22:58Mji mkuu wa Niger, Niamey, unashuhudia vuguvugu na taharuki kubwa ya jeshi na wananchi wanaowaunga mkono viongozi wa mapinduzi wakipinga uwezekano wa uingiliaji kijeshi wa nchi wanachama wa Jumuiya Kiuchumi ya Magharibi mwa Afrika (ECOWAS) nchini humo.
-
Zakzaky: US, Ufaransa zinataka kuibua uhasama baina ya Nigeria na Niger
Aug 19, 2023 07:00Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria (IMN) ametahadharisha juu ya njama na majungu yanayopikwa na Marekani na Ufaransa ya kupanda mbegu za chuki, uhasama na mifarakano baina ya Nigeria na jirani yake Niger.