-
UN: Watu milioni 14 watahitajia msaada wa dharura Nigeria 2017
Nov 16, 2016 10:46Umoja wa Mataifa umesema watu milioni 14 watahitajia msaada wa dharura mwaka ujao wa 2017 kaskazini mwa Nigeria na kwamba makumi ya maelfu ya watoto wapo katika hatari ya kupoteza maisha kutokana na njaa katika eneo hilo ambalo lilikuwa ngome ya kundi la wanamgambo wa Boko Haram.
-
Wanafunzi elfu 80 kuacha shule kutokana na njaa Zimbabwe
Oct 19, 2016 11:58Wanafunzi zaidi ya 80,000 nchini Zimbabwe wapo katika hatari ya kukatiza masomo yao kutokana na baa la njaa ambalo limefikia "kiwango cha kutisha."
-
UN: Watoto 75 elfu wapo katika hatari ya kufa njaa Nigeria
Sep 29, 2016 10:24Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuwa, maelfu ya watoto wadogo wapo katika hatari ya kupoteza maisha katika kipindi cha mwaka mmoja ujao, kutokana na njaa na utapiamlo 'uliosababishwa' na kundi la wanamgambo wa Boko Haram.
-
UN: Wakulima milioni 23 wanahitajia msaada kusini mwa Afrika
Jul 28, 2016 23:46Umoja wa Mataifa umesema wakulima milioni 23 katika nchi za kusini mwa Afrika wanahitajia msaada wa dharura kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao wa upaliliaji.
-
UNICEF: Watoto elfu 49 wanakabiliwa na utapiamlo Nigeria
Jul 20, 2016 02:56Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF umetahadharisha kuwa, watoto 49,000 wako katika hatari ya kupoteza maisha kutokana na baa la njaa na utapiamlo nchini Nigeria.
-
Watu karibu laki sita wanakabiliwa na baa la njaa Angola
Jun 02, 2016 23:23Umoja wa Mataifa umeonya kuwa watu laki tano na elfu 80 wako katika hatari ya kupoteza maisha kutokana na baa la njaa nchini Angola.
-
Watu milioni 8 wanahitajia msaada wa chakula Malawi
May 25, 2016 23:56Serikali ya Malawi imesema kuwa, zaidi ya watu milioni 8 wanahitajia msaada wa chakula nchni humo.
-
Msalaba Mwekundu: Watu milioni 31 wanahitaji misaada ya dharura kusini mwa Afrika
May 17, 2016 23:03Mashirika ya Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu yamesema yanahitaji dola milioni 110 za Marekani ili kuzisaidia nchi za kusini mwa Afrika, zinazokabiliwa na hali mbaya ya ukosefu wa chakula na lishe duni iliyosababishwa na ukame.
-
Madai ya serikali ya Msumbiji kuhusu usiri katika deni la nchi hiyo
Apr 29, 2016 23:43Waziri Mkuu wa Msumbiji amesema kuwa, machafuko nchini humo ndiyo sababu kuu iliyoifanya serikali kuamua kuficha habari kuhusu deni la dola bilioni moja na laki nne la nchi hiyo kwa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa IMF.
-
Umoja wa Mataifa: Watu milioni 30 barani Afrika wanakabiliwa na ukame na baa la njaa
Apr 17, 2016 02:37Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, ukame na baa la njaa linatishia maisha ya watu milioni 30 barani Afrika.